Ile kasumba ambayo mimi naona ni ubinafsi au kutafuta/taka kuonewa "huruma".....yaani marehebu baba blablabla....Marehemu sijui nani blablabla. Marehemu Baba wa Taifa anatuangalia na kugalauka Kaburini......yaani aache kufanya yaliyomuhimu huko aliko abaki kutuangalia sisi huku na kugalauka kutokana na ujinga au makosa na shida zetu!
Sidhani kama hao marehemu huwa hata wanatuombe tulio hai tuendelee kupata "kiza" cha milele ili tusiamke na kukabiliana na shida za Dunia. Mtu akienda, ameenda na huna budi kukubali kuwa kaenda na anaendelea na maisha mengine bila wewe....dizaini ukifa unasahau all bout Dunia na watu wake.....Mambo ya new start...new life.
Si wanasema unakuwa "declared dead only" kama Ubonko (Ubongo) haufanyi kazi, sasa kama Ubonko haufanyi kazi kumbukumbu za ya Duniani watazitoa wapi? (In my head). Usikute Baba yangu kaoa mke mwingine na anawatoto huko wanasoma Shule "international Academia" wakati mie alinipeleka Shule za "Msondo"....nani ataka upweke hapa Duniani....oh kule sio Duniani....aah well!
Muhimu ni kutotaja taja marehemu kila unapokuwa na mashida na mahuzuni yako, "mama angekuwa hai angenishauri"....."Baba ataniongoza tu kwenye hili".....wao hawawataji wana-deal na yao huko waliko. Duh! Baba yangu ni marehemu....hii "Marehemu Baba" haizoeleki....maskini angekuwepo angecheza na wanangu.
Takuona J'3
Kwaheri kwa sasa...
Mapendo tele kwako...
Comments