Skip to main content

Posts

Showing posts with the label blog za tanzania

Diaspora Wives...

...the long suffering ones wa US, UK and Canada nyie wa Scandinavia, Spain, Italy, Germany, etc hamuolewagi...wait, huwa hamuolewi na Waafrika wenzenu na wengi ni Mama wa nyumbani (natania). Dayaspora wives work several  shifts in the cold and spend the  money to support their husband's  business ventures in Africa. Them ones who want something back home, they want to become somebody somewhere kule kwa Motherland.  Mnakubaliana vema tu kuwa mara 4 kwa mwaka yeye atakuwa anaenda Tanzania au Kenya(depends on their origin) na kukaa huko kwa wiki 2 mpaka mwezi "kusimamia" Mradi/Biashara,  hiyo ni kila baada ya miezi 3.                                       picha kutoka gazeti la The Telegraph*? Kwasababu ya yeye kurudi kwao/kwenu mara kwa mara ni wazi kuwa haingizi kipato cha kutosha na hivyo yeye sio breadwinner isipokuwa wewe mkewe. Unajitolea mhanga ukiamini kuwa Mradi ukikamilika utaacha kufanya kazi kwa kiwango ufanyacho na Mumeo kuwa breadwinner, a provider

Enzi tulitongozwa uchochoroni...

Miaka 10 iliyopita mlitongozana kwa texts au kwa sauti baada ya kuona picha, nasikia siku hizi wala hamtongozwi kabisa au nyie ndio mmekuwa watongozaji. Wanawake wamekua wawindaji, watafutaji, wapiganaji....wanaume wanafanya nini?  Basi sie "Mid Gen X" a.k.a Xennials a.k.a MillenX (tulizaliwa 1975-85) tulikuwa tunakimbiliwa huku tunaitwa " oyaa mrembo" au "oyaa dada'ke (weka jina la kaka yako)" au hey Binti (weka jina la Baba yako), kama jamaa humtaki/hakuvutii unakimbia kama athletes au unaingia kwenye nyumba yeyote unatulia mpaka jamaa apitilize au ageuze na kurudi kijiweni, then unaendelea na safari zako au inatokea mtu kwenye nyumba hiyo anakisindikiza so unakuwa pretected. Kama jamaa unamkubali basi unapunguza mwendo so anakufikia haraka.  Mnatembea huku anakuuliza maswali kisha mnafika kichochoroni(hakuna watu wengi) then anashusha mistari yake...unadengua-dengua pale na kujiringisha(hiba ya kike) huku unachora chini au unatafuna kucha...unamuang

Asking for money, mmepoteza aibu online?

Majuzi nilikuwa nakatiza mitaa ya YouTube  nikitafuta best  Female TV talk show Bongo Tanzania baada ya kukumbuka enzi nikiwa msichana kulikuwa na kipichi cha wanawake, siku mbuki jina wala Host wake ila Jaquline Ntuyabaliwe (sasa Mrs Mengi) alikuwa mshiriki, ilidumu kama episodes 3 hivi(kila Ijumaa/Jumamosi)..unfortunately sikupata nilichokuwa natafuta ila  nikakutana na podcast/Youtube Channel ya Salama, nikawa nasikiliza mazungumzo na mgeni wake, which was quite interesting then kwa chini I saw there were kijibango anaomba "kuchangiwa" as in donate to the channel/podcast, I thought these people have no mshipa wa aibu.  Am used to other youtubers asking for money or as they demand "cash Up me:, "donate first ndio nitaanza kuongea", "join my channel  for elfu 3(£1) kwa mwezi to get exclusive"...but Dada si Muajiliwa kule Sekta ya private which they pay better than Serikalini...No? au mazungumzo yake na Mastar ni side haso?  Huwa najiuliza, I (you) su

Endelea mtongoza Wife...

Ni kawaida kwako Mume (na jamii kwa ujumla) kutegemea mkeo afanye kila awezalo kuifanya ndoa kusimama utasema kajioa mwenyewe. Kuna siku nikaamua kugugo matatizo ya Ndoani, kila maelezo niliyoyapata kwa Kiswahili na Kiingereza, mzigo wa kuweka mambo sawa wenye Muungano huo alibebeshwa mke.   Hakukua na maelezo ya kutosha ambayo yanamsaidia Mume kutatatua matatizo ya ndoa zaidi ya nini afanye akishindwa kusimamisha, Mke na Mama nani nimpende? au nini cha kufanya ikiwa anamaliza haraka? Vipi kuhusu nini cha kufanya ikiwa umemuudhi mkeo? Nini mbadala wa kumnunia/fokea/ignore mke wangu, kitu gani nifanye kukabiliana na mzunguuko wa hedhi wa mke wangu baada ya kupevusha pale anapokaribia Siku zake(sio za kufa bali Hedhi) n.k.? Kuna mengi kwenye ndoa zaidi ya Ego, Mama yako na Uume wako.     Kwenye blog hii tutakumbushana mengi tu ambayo hayahitaji uekisipati wa jinsia bali ni uelewa wa kawaida tu wa kusomana kwa pande zote mbili. Nakumbuka enzi nilipokuwa Twitter kuna wakaka wawili nawahesh

Saikolojia ni Sayansi rahisi, you need to heal...

...huwa wanamaanisha nini? ku-heal ndio kukoje wakati huna matatizo ya kiafya(kimwili)?  Kuna maneno watu wa mitandaoni wanapenda kuyatumia ili kuonekana wajuzi au wana upeo ama wana akili/wasomi(kila mtu anataka kuonekana hivyo), unakuta mtu anajieleeeeeza halafu hakuna anachoelezea, anajazia tu maneno ambayo yana-sound vizuri au kisomi ama yale "clinical" yanayotumiwa zaidi ya Wanasaikolojia(wale wenye Leseni ya kutoa Huduma hiyo baada ya kumaliza masomo na kufuzu kwa kiwango cha phD) au Madaktari wa Akili Sisi tuliosoma "Social Science" kama sehemu ya Kozi nyingine hatupaswi ku-act kama vile ni Wanasaikolojia, ni kama Sheria kuna sehemu unaijua na unaweza kuizungumzia lakini wewe sio mwanasheria, uliisoma tu kama sehemu ya Kozi yako na sio Kuisomea. Huezi amini leo ndio nimeelewa kwanini Wanasheria wa Bongo huitana "Mwanasheria Msomi". Juzi hapa nilikuwa nasikiliza PodCast(yeah them ones) kuhusu malezi ya watoto kutoka kwa "wataalamu", kukawa

Tangu umefunga ndoa, ume-improve...

 ..Mchezo au upo vile vile? Kwamba ya nini ni-showcase  au ujiboreshe wakati  umeshampata, ni wako mpaka kifo? Sio sasa ni wangu wacha ni practise nae zaidi na time to time ni showcase niliyofuzu? nayo hapana? Ndoa ikibuma je utaanza kujifunza upya?  hehehehe hawa wa siku hizi hawajui kusubiri, yaani hata muda wa ku-show off maujuzi hupewi.....ukitoka na hujalipia  meal, umeachwa(wakati haukuwa na uhusiano nae)....hii kwa wote, wewe na mkeo/mmeo.  Natambua kuna kubadilika au tuseme kukua(inategemea na umri mliofunga ndoa)....uboreshaji  wa tabia au mtindo wa maisha ni jambo muhimu, maana huwezi kuishi kama kijana/binti wa miaka 32 wakati sasa una miaka 47...Wataalamu wanasema kuwa Uhusiano haubadiliki bali wenza ndio hubadilika, mimi nabisha kwasababu ninyi mkibadilika/kua ni wazi kuwa mahitaji yenu yanabadilika na hivyo uhusiano mzima kubadilika.  Mfano; Uhusiano wenu ulivyokuwa kabla ya kufunga ndoa ni tofauti na sasa mmefunga ndoa, na uhusiano huu baada ya ndoa hubadilika baada ya k

Twitter ya Elon na heka heka zake...

Ni mwaka na wiki kadhaa tangu Elon Musk alazimishwe na "Mahakama" aichukue Twitter  baada ya kutishia kuinunua 2021(for attention) na ni Mwaka  Mmoja na Wiki Sita tangu nami niachane na Twitter(nisome  kama unajali  ). Maisha bila twita yamekua ya kwaida na sijawahi kuhisi kutamani kuchungulia na kusalimia watu wangu ambao huwa  nawakumbuka mara kwa mara na kutabasamu kutokana na vichekesho au jinsi tulivyokuwa tunaelewana, kupishana na kushangaa pamoja. Hey I miss you on twita too. Sasa juzi hapa nikaona habari kwamba Elon anataka kubadilisha Kindenge na kuwa Eksi(huenda tayari imekuwa hivyo), nikaudhika na kuombea Twita ikufe kabisa na kubaki kumbukumbu, maana ni aibu hata kusema niliwahi kuwa Twita tangu mwanzo miaka 17 iliyopita. Ilikuwa jamii nzuri sana na kamwe sitoisahau kama ilivyokuwa DHB(Dar Hot Board)/DHW(Dar hot Wire), JamiiForum na Facebook. Nimesikia kuna mabadiliko mengi ambayo nilijua yatatokea kutokana na jinsi Elon anajibeba. Elon ni Bilionea amb

Jinsi ya kurudisha furaha kwenye Ndoa yenu!

Kumbuka sababu kuu ya ninyi kuwa pamoja ni mapenzi na sababu ya kufunga Ndoa ni kwavile mnapendana na mnataka kuishi pamoja kwa furaha. Ulipenda na ukataka kupendwa na kufurahia Muungano wenu. Sasa kama hiyo ndio sababu kuu, kuna umuhimu gani wa kuendelea kuishi Maisha ya ndoa wakati hakuna furaha? Utasema Mapenzi, kwasababu mapenzi hayaishi obviously, jinsi mnavyozidi kuishi pamoja ndivyo ambavyo unapata sababu nyingine nyingi kwanini unapenda Mume/Mkeo.   Kuna wakati unaweza usipendezwe na mumeo/mkeo kutokana na matendo yake au kutokana na jinsi alivyokujibu/ongea nawe au kafanya jambo Fulani hukubaliani nalo, hii hali hutoweka mara akiomba radhi au wewe ukiamua kudharau. Hali hiyo haiondoi mapenzi yako kwa mume/mkeo.   Ule msemo wa watu wa social media kuwa “my happiness comes first” au “I choose me” ni kwa wale ambao hawana Imani (hawamuogopi Mungu) ni single au wapo kwenye Ndoa mbaya za unyanyaswaji, vipigo, mateso na masimamngo. Sie wengine ambao wenza wetu wamebadilika sab

Kufananisha/linganisha relationship...

 ,,,au yaliyopita si ndwele tugange ya jayo? Ikiwa umetoka Kimataifa (mbali sio nchi za jirani) halafu baadae ukajaribu nyumbani na kubaki huko kimapenzi ili kuepuka kufuta Race ya watu weusi unakuwa na uzoefu tofauti au tuseme kacha ya kupendwa na kujaaliwa na akupendae tofauti kabisa. Ni kama vile mategemeo yako(maisha uliyozoeshwa) yanakuwa hayana nafasi, sometimes unaeza  jaribu kuyafanya wewe badala ya ku-receive ukitegemea mweza atakusoma ili akupe upatiacho? unatoka bila. Mwanzoni kabisa unaeza usijali sana kwasababu penzi ni upofu obviously, ila jinsi mahusiano yanavyozidi kukua nakuota mizizi unaanza kugundua kuwa watu wa nchi za mbali wanajali zaidi na wanaonyesha mapenzi zaidi kuliko wa nyumbani(inawezekana wanaogopa kuonekana wabahuzi). Kwa kawaida unaambiwa usifananishe/linganishe ila kama ulikotoka huko Mataifa ya mbali kulikuwa ni furaha  na "kula bata" zaidi ya maumivu kihisia na huzuni...unajikita tu unarudi na kuanza kukumbukia(hulinganishi bali unakumbukia)

Chochote ukijuacho/ulichopitia make money out of it...

 ...uza uzoefu wako iwe wa mapenzi, magonjwa, uzazi, matatizo ya familia au hata disoders na matatizo ya akili! Mie sikujua kama kuwa home body(which I am) ina jina lake na kuna watu wanatoa "courses" kuwafunza wenzao ambao nao ni introverts(hawapendi watu wala kujichanganya nao kwa zaidi ya lisaa limoja) namna ya kuondokana na hali hiyo. Hakuna mtu anaweza kubadilisha vile ambavyo umeumbwa....kuwa mwenye aibu, mapole, mkali, mtembezi, mpenda ku-party, usiopenda ku-party n.k. binadamu tunatofautiana na that is okay. Sio sahihi kutumia "kipaji" ambacho honestly huna na hata kama unacho sio muhimu na hakina faida kwa yeynote Duniani halafu ukaanzisha Kozi ili uweze kuwa tajiri, kwanza kwanini unataka kuwa tajiri? na ikiwa kuwa tajiri ni rahisi hivyo kwanini wengi wetu sio matajiri? Kuna ubaya gani kuingiza kiasi cha kutosha kuendesha maisha na kufurahia Holiday na kumaliza matizo yako ya kifedha mwenyewe bila kuwa tajiri? you know, kufanya kazi na biashara pembeni kih

Mind your Ughaibuni business...

 Nakumbuka miaka michache nyuma nilipokuwa Twita alijitokeza Binti mmoja nakuanza kuwaambia watu wa Ughaibuni(Nchi za Ulaya na Marekani) kuachana na Siasa za Tanzania na kufurahia maisha yako "mazuri" popote walipo Ulaya(popote nje ya Afrika)....natabua kua sio kila mtu Ulaya ana maisha mazuri(inategemea sababu yako ya kuishi huko) lakini nakubaliana nae. Wabongo wengi walimkandya/ponda kwa kudai kuwa anataka attention ya Bongo Twita sababu hakuna mtu anamfahamu, binti alijitetea na kusimamia alichokisema ambacho hakika nakubaliana nae. Watu wa Ughaibuni ambao hawaishi Tanzania  wanaguswa na Mabadiliko ya kisisa yanayoendelea Tz, hawa ni wachache sana ambao wana Biashara na pengine kumiliki ardhi(nyumba, mshamba n,k,) na wachache ambao hurudi nyumbani mara kwa mara, wengine wapo wapo tu na ndio huwa na kelele zaidi kuhusu Tanzania na Siasa zake. Unadhi utabadilisha nini  Tz na Kodi hulipi? Mind your Ughaibuni business and enjoy your High tax, cost of living and free Heathcare

Kila Familia/Ukoo ina mtu huyu...

  ...Kikao cha familia, hakianzi mpaka Dada/Kaka aje... Kwenye kila familia (hasa kama mpo wengi) huwa kunakuwa na ndugu mmoja ambae anajipa cheo na anataka abaki pale kwa njia na namna yeyote ile. Achana na wale ndugu wakubwa ambao automatically wanapewa "uongozi" na Wazazi...kuna yule mmoja wenu huibuka tu na kuanza kujiona ndio mwenye akili, ndio fashionable, Mfuata maadi, anajua kila kitu maishani, anafahamiana na watu wenye Majina(maarufu/viongozi), Msomi n.k, mara nyingi huwa mtoto wa Tatu mpaka Tano hivi kuzaliwa. Huyu mtu huangalia mapungufu kwenye familia halafu ana pursue kitu ambacho kitamfanya awe tofauti na ninyi wote. Kama ni Elimu basi atasoma kwa bidii na juhudi zote ili awapite wote, kama  ni mafanikio kiuchumi atakuwa juu zaidi ya wote humo familiani(hii itampa nguvu ki-social hasa kwenye mikutano ya familia), likija suala la marafiki, yeye atakuwa ni rafiki zaidi kwa marafiki zenu wote ila rafiki zake ni wake peke yake...kwenye suala la wanawake/wanaume(ina

Mtoto wa kambo...part 2.

Mtoto wa kambo...part 2. Ukiachana na misukosuko ya txt na simu za mama mtoto, kuna suala la kufanya mapenzi ambalo wengi huwa hawalizungumzii sababu wanaogopa kuambiwa hawajiamini. Unless wewe una-elements za kichawi au zile za ukimada ndio utaweza kuwa na a very good sex life on the daily (kila anapowasiliana na mkimama wake wa awali kabla yako, unapata mhamko).   Vinginevyo bana the thought of dudu kuingia kwa mwanamke mwingine bila kinga itakuondolea hamu na ile desire kwa mpenzi wako inatoweka, unaanza kujiambia “omg nimekosea kuchagua”, kama umeshawi humuona ex unaanza kujiuliza kama jamaa ana type na wewe umefanana na Ex wake, unapata kinyaa…unawaza “niingie mitini nini?”, unaendelea kuwaza “yaani ndio nimejitolea mhanga maisha yangu yote yatakuwa kupambana na drama za ex”, “si bora niwe single and happy” …yaani akili haitulii. Na kama ujuavyo bila akili kutulia, hakuna ushirikiano na bila ushirikiano tendo hakuna, ukifanya linakuwa doro.     Kwa uzoefu wangu na wenetu wat

Mtoto wa kambo(part 1)...

Mtoto wa kambo sehemu ya kwanza.... Kambo maana yake nini? Ikiwa mtoto alizaliwa nje au kabla ya ndoa nae anaitwa mtoto wa kambo? au ni kwa wale waliozaliwa ndoani halafu  ndoa ikafeli au mzazi mmoja kafariki halafu  baba/mama kaoa/olewa tena?  Mnaona mlivyo haribu/changanya mambo baada ya kuua umuhimu wa ndoa na kujenga familia? Mtoto kabla na nje ya ndoa (Wanaharamu) huwa hawajulikani/hawana umuhimu(kwa Waislamu hii bado imesimama). Nimekukwaza? ndio ukubwa huo.😁 Mama/baba wa kambo inatumika zaidi Mikoani, huku kwetu Pwani tunatumia sana Mtoto wa kufikia(kwamba umefika   kimapenzi kwa mwanamke/mwanaume ukamkuta mtoto kutoka ndoa iliyopita?)…sina uhakia. Nitatumia maneno mtoto na watoto interchangeably. Nani alipitisha sheria ya kulazimisha watu wawapende watoto waliowakuta kwa watu waliowadondokea kimapenzi? Yaani ukionyesha huna habari na uzao wa mwanamke/mwanaume kabla yako basi unaitwa Mwanga, unaroho mbaya n.k. Utapendaje mtu wala humjui na hana faida kwako?  Natambua kuna msemo

Huge Microphones na yupo youtube...Kero zangu.

...ndio mnaita podcasts?  wameharibu youtube eti, au nimezeeka niachane nayo kama nilivyoiacha twita? Anyways, hujambo? Unaendeleaje na u-pre-menopause? Kama binadamu hakika kuna vitu vinakukera, binafsi nakwerwa na sehemu kubwa ya jamii ya online, hasa mamilionea na wamarekani weusi wanaoijua Afrika na kacha zake zote (nchi 57?) baada ya kwenda Ghana kwa wiki moja wa youtube na mi-microphone yao makubwa ka' wapo Mawingu FM. Halafu usinikumbushe wale wanajipanga kwenye vibox(zoom meetings) wanaanza kubishana oh my days.,,,ukute ni wivu wangu tu, maana  wanangu wakienda shule na Baba yako Kazini nabaki hapa sina hili wala lile. Ukiachana na hao kuna wale young single men and women wanashauri/fundisha wenzao namna ya kuishi maisha ya ndoa(Well I did that when I was younger but kama unakumbuka nilishauri kuhusu mahusino na ngono nilikuwa in one na was doing it). Najua unatambua kua sio tu Ndoa ni tofauti na maisha ya ndoa, pia Ndoa sio mahusiano japokuwa mahusiano ni sehemu ya ndoa. N

Bichwa kubwaaa tiny brain......

Women....sio kwamba tuna mabig head bana ni nywele tu hizo. ...Pia hatuna tiny Ubongo isipokuwa sehemu kubwa ya Ubongo wetu inatumika. Yaani tunatunza mambo mengi sana na hufanya tuwe na kumbukumbu nzuri kuliko wenzetu.... si wajua Data zikikaribia kujaa kwenye PC au Simu which is PC. ...isn't it?.....speed inapungua. Unajikuta unakuwa mvivu kufikiria kwa undani kabla hujasema matokeo yake unatoa lolote halafu unagundua neno likitoka halirudishiki.....unabaki kujuta au ku justify. Wanaume ambao walikaribia wanawake ni wale waliotumia 1/3 ya Ubongo wao na baadhi yao ni JK Nyerere, Gandhi na B Mkapa(no Nkapa really I just liked him as prezzo). Kama hutaki kuamini nikuambiacho kuhusu matumizi yetu ya Ubongo nenda kaGUGE. (Googling......kaguge usisahsu you heard it here 1st). Binafsi huwa nafikiria huku naongea au kuandika na matokeo yake huwa si justfy bali nasimamia nilichokisema na kukusaidia kunielewa. So wacha uvivu, soma magazeti ambayo ni broadsheet sio tabloids. ...wacha bl

Kabla hujafa, hujaumbika!

Ni kawaida ya watu (wengi) kucheka matatizo ya wenzao au kuyazungumzia katika mtindo wa "kichekesho". Mimi napenda sana kucheka na kuchekesha (japo kuwa sichekeshi....yaani nikitoa kichekesho watu hawacheki mpaka nielezee kwanini nilichosema kinachekesha)....hihihihi achana na hili! Matatizo nayogusia hapa ni yale ambayo mtu hana uwezo wa kuyazuia, sio matatizo ya kujitakia(kuchagua) kama vile Utumiaji wa Madawa (japokuwa hata hawa mie huwa siwacheki). Kama huna utu na huna mpango wa kumsaidia mwenye matatizo kwanini uzungumzie matatizo yake kwa watu wengine katika hali ya "kumcheka"? Wengine wanapoleta habari za mtu za kusikitisha kutokana na matatizo yake yaliyobadilisha Mwili au Akili (Ulemavu) yake hawacheki kwa kukenua Meno, lakini jinsi wanavyoelezea unagundua kabisa wanamcheka mhusika. Mf; "Eh bwana unamkumbuka Elia? Daah jamaa yaani kaisha halafu sasa anatembelea Mgongo. Yule jamaa alikuwa anajifanya mjanja sana"....umeona? Hakenui meno laki

Marehemu....

Mungu aendelee kuwapa Mwanga wa Milele, Amina......hebu ngoja kwanza!! Wameenda wakiwa "wamelala" sasa mwanga wanini wakati wamelala? Ile kasumba ambayo mimi naona ni ubinafsi au kutafuta/taka kuonewa "huruma".....yaani marehebu baba blablabla....Marehemu sijui nani blablabla. Marehemu Baba wa Taifa anatuangalia na kugalauka Kaburini......yaani aache kufanya yaliyomuhimu huko aliko abaki kutuangalia sisi huku na kugalauka kutokana na ujinga au makosa na shida zetu! Sidhani kama hao marehemu huwa hata wanatuombe tulio hai tuendelee kupata "kiza" cha milele ili tusiamke na kukabiliana na shida za Dunia. Mtu akienda, ameenda na huna budi kukubali kuwa kaenda na anaendelea na maisha mengine bila wewe....dizaini ukifa unasahau all bout Dunia na watu wake.....Mambo ya new start...new life. Si wanasema unakuwa "declared dead only" kama Ubonko (Ubongo) haufanyi kazi, sasa kama Ubonko haufanyi kazi kumbukumbu za ya Duniani watazitoa wapi? (In my