Skip to main content

Wenye Ndoa, tuache kuwabadilisha Waume Zetu.



Sasa kabla hatujaanza kumsimamnga Wifi kambadilisha Kaka yetu, tuangalie kwanza Wifi alikuwa nani kwao, na je uamuzi wa Wifi kupumzika ki-career baada ya Kuzaa ni kum-support Kaka yenu(Mumewe) ki-career au ni njia tu ya yeye kula Mahela ya Kaka yenu? Je ndugu zake waliokuwa wakimtegemea hawateseki kwa kukosa "kipato" kutoka kwa Dada/Mwana wao?



Kwenye era hii ya Sosho Midia inabidi uwe makini sana maana info ni za kumwaga(tofauti na 2007 nilipoanza  kublog), ni kweli baadhi zinasaidia hasa zile za Medical kutoka kwenye Site za Shirika la Ugojwa husika au Shirika la Afya Duniani. Lakini linapokuja suala la Ndoa au mahusiano, ongeza umakini kwasababu Ndoa hazina Kanuni Moja na watu hatufanani hata kama tulikaa tumbo Moja Miezi 9 na kuzaliwa kupitia Njia mooja na siku Moja bado tutatofautiana kwa kiasi fulani.



Maisha magumu, kila mtu anatafuta views na clicks siku hizi, mara zote(kama Wanasiasa) watu huamua kuongea au kuandika mambo ambayo wanajua watu watakuja mbio kutaka kuona/jua. Labda ni kwavile ndio wanachopitia hivi sasa au wanajiandaa just incase ikitokea watakuwa wanajua namna ya kupambana.



Siku moja "nilitumiwa" Video ya Mwanamke(as you do) akiwaasa  Wanawake kama yeye kutowabadilisha Waume zao na kukamata Pesa zao na hivyo Waume hao "kusahau" Familia zao. Nikaendelea kusikiliza nikiamini kuwa anawazungumzia Vimada in which nilianza kumuunga Mkono.


Baadae akasema "utakuta Umeolewa na Mwanaume ambae alikuwa anategemewa na familia yake, lakini baada ya muda unambadilisha Mumeo na kuitelekeza Familia yake. Familia  yake inateseka kwa ajili yako. Familia uliyomkuta nayo, iliyomlea, tuache kuwabadili Waume zetu". mmmh!


Nikajisemea "huyu Dada lazma hajasoma (hana Elimu ya juu) au ameolewa akiwa hana Kazi wala Majukumu kwenye Familia  yake(Wazazi na Ndugu zake). Kuna akina sie ambao tulikuwa tunategemewa pia na Familia zetu, mpaka baada ya Kuzaa na Waume zetu. Je kuna mtu anaenda kueneza "Neno" kuwa Waume zetu wasitubadilishe Wake zao?



Wazazi wetu (sisi Wake) hawakutumia Pesa zao kutusomesha na kutupa maadili mema ili tuje "kuzalishwa" a.k.a "haribiwa shape" na kuacha Career zetu kwa Muda ili tulee watoto ambao wanabeba Jina lenu la Ukoo. Hebu wekeni Heshima, ebo!



Sijawahi kusikia mtu yeyote akilalamika kuwa Wake tumebadilishwa na Waume zetu baada ya kufunga nao ndoa, sio kwamba "hawatubadilishi" la hasha! tunabadilishwa pia.....tena sio kubadilishwa hehehehe, tunaharibiwa Shape na isitoshe kupatwa na Maradhi ya ajabu ajabu for the rest of our lives.



Sidhani kuwa tunawabadilisha Waume zetu, bali Majukumu na Vipaumbele vinabadilika. Watoto na Mkewe wanakuwa muhimu zaidi kwake kuliko Ndugu zake. Ndugu zake wamekua/watakuwa na maisha yao bila yeye. Yeye hakuwaleta Ndugu zake Duniani bali Wazazi wenu, kama yeye alivyo Mzazi kwa Watoto wake.



Kuna wakati Maisha hubadilika(mtu unakua mtu Mzima), Familia yako inakuwa Wewe, Mkeo/Mumeo na Watoto wenu. Wale mliozaliwa pamoja kama Familia mnakuwa sio "Familia" tena, mnabaki kuwa Ndugu wa Damu. Upendo na uzito/umuhimu upo  pale pale, mtasaidiana ktk shida na mtatembeleana lakini hauwezi kuwa Tegemeo lao Kiuchumi.



Sawa, huyo ni Kaka yenu ambae ni Mume wa Mtu mwingine(Wifi yenu), mnamjua Kaka yenu tangu utoto wake lakini Mkewe anamjua Kaka yenu  katika Kiwango kingine tofauti na cha kipekee ambacho hata mfanye nini hamuwezi kumjua kihivyo(sizungumzii Ngono hapa), sio nyie tu  Ndugu zake bali hata Baba na Mama yenu.


Nathamini muda wako hapa, shukrani kwa kunichagua Mie leo.
Noo see ye efter.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao