Skip to main content

Wanawake hatupendani....usimbee awe Jaji sasa!



Sina hakika kama hii ni Imani tu au ni kweli, Naturally Wanawake hawanipendi mie binafsi(imagine ningekuwa mzuri sasa!) ila Wanaume wanananipenda(napatana zaidi na Wakibaba kuliko Wakimama). Kuna siku Mfanyakazi mwenzangu akanijia kwenye Dawati langu akanambia "dinah unajua nakuchukia".....mie nkacheka halafu nikamwambia "sio peke yako, nimezoea kuchukiwa na wanawake"....wewe ungesema is because i am Black!





Sasa, hii "wanawake hawapendani" ipo kila Nchi Duniani.....kila mtu anaibuka na sababu yake kwanini hasa hatupendani. Baadhi wanadai ni Wivu wa kike(umbile/kupendeza/mafanikio/kuwa na easylife) na wengine wanasema ni mambo ya Homono tu.





Mie sio kwamba nachukia wanawake bali sipendenzwi na tabia ya baadhi ya wanawake wanaofanya maamuzi ya Kipumbavu, kama vile kutojikinga dhidi ya Mimba, au kujitegeshea kushika Mimba ili tu waolewe au wapate sehemu ya Kipato ya Mwanaume husika. Sipendi mwanamke ajishushe ili kuonewa kirahisi.




Vilevile nachukia wanawake wanaokandamiza wanawake wenzo kutokana na masuala ya kike ili tu waonekane Imara. Unawajua wale wanaoamini kuwa Mimba sio Ugonjwa? au Mwanamke asipozaa basi sio Kamili? ama Mwanamke umeumbwa kuzaa? The shenzi kabisa.




Kutokana na Wimbi kubwa la watu kuachana, kumekuwa na Kesi nyingi kutoka kwa Wanawake wakidai Baba wa watoto wao kuwatunza wao na watoto wao. Hizi Kesi zinaweza kuwa Complicated (inategemea na chanzo cha kuachana, asili ya uhusiano, Umri wa Uhusiano na Mali mlizokusanya mlipokuwa pamoja n.k).




Lakini Majaji wengi wa Kike(Wanawake) wamekuwa wakilaumiwa kuwa na Chuki dhidi ya Wanawake wenzao kwa sababu hawaruhusu Wanaume kutoa pesa za kutosha kwa ajili ya watoto na wao(mamaz). Wanawake wanaamini kuwa kulea watoto ni kazi ngumu (nakubaliana na hili) na hivyo kama Baba hayupo "kimwili" basi Mfuko/Bank acc yake inapaswa kuchangia "ugumu" wa kule watoto wao.




Wanawake wengi wanaegemea zaidi kwenye Chuki "asilia" ya wanawake kwa wanawake. Mie nasema sio chuki bali Wanawake hao(Majaji) wanajaribu kutoa ujumbe(wengi hutoa somo mwisho wa Hukumu) unaofanana na, acha uzembe wa kutaka kutunzwa (via pesa zake) na mwanaume ambae hapati "matunzo" kutoka kwako(ni Ex) na badala yake nenda katafute pesa zako ujitunze mwenyewe.




Sawa, Watoto wana Haki ya kutunzwa/lelewa na wazazi wote wawili wenye Mapenzi sawia(au zaidi kwa one another) lakini likitokea la kutokea au in your case(sorry hihihihi) ulijitegeshea basi usitegemee kuishi kwa kutumia Kipato cha Mwanaume ambae hayupo nawe.





Majaji wengi wanawatoto na hakika walichukua muda kulea watoto wao walipokuwa wadogo kisha wakarudi  Kazini/Shuleni. Wengine walisaidiwa na Walezi kwenye Vituo vya kulelea watoto iwe Nursery au Nyumbani kwa mtu au kwa Ndugu na Jamaa. Hakika hii ni personal choice, lakini kama wao waliweza kufanya hivyo kwanini wewe ushindwe?





Weka mfano mzuri kwa kwa Watoto wako kuwa wewe  ni Mama Imara na huitaji Mwanaume ili kuishi/kujipenda/kupendeza/kuvutia/kujenga. Muonyeshe Ex wako kuwa Unaweza kuishi Maisha Bora zaidi bila yeye.


Ahsante kwa kuichagua Blog hii.
Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao