Skip to main content

Hebu tuone Past life yako: Kutelekezwa/Achwa...

Umekuwa na mama yako kwa Miezi 9 mpaka 11 kama ulikuwa na bahati, wengine ni miezi 6 na wengine karibu Mwaka(Miezi 12).



Ni mtu pekee unaemfahamu, na unahisi kuwa upo salama na unapendwa, sababu Mtu huyu sio tu amehatarisha maisha yake ili kukubeba na kukuleta Duniani. Mtu huyu ataendelea "kuteseka" sababu unataka ule x4 usiku wa manane, ataendelea kukupenda, kukulinda, kukufunza na kukujali. 



Hayo yote hutokea kwa Miezi 3 ya mwanzo, baada ya hapo unamuona mtu huyo Nusu siku, kila unapoachwa unalia sana. Siku zinavyozidi kwenda ukaribu wako na mtu huyo unapungua na kilio chako kinapungua.



Kitendo cha Mtu huyo ambae sasa unamtambua kama Mama(au Anty, Dada wa Kazi ndio Mama yako) kukutelekeza/kukuacha huwa kinaumiza sana.



Sasa umekua na unajitegemea kwenye mambo mengi kama vile kucheza peke yako, kujivisha viatu/nguo nk. Lakini bado ni Mtoto na bado unamuhitaji Mama yako.


Jana la leo Mama amekua nyumbani siku zima, unahisi furaha, upendo na kujaaliwa.....Mama anaamua kutaka kutoka kidogo, anaanga, wewe unaanza kumlilia. 



Mama anasema "nenda kavae Viatu twende"...unatoka mbio kuwahi Viatu...ile umefika alipokuwa Mama anakusubiri, hayupo. Kakuacha/kakutelekeza na hujui kaenda wapi. Unauliza mama yuko wapi? Wanakuambia hawajui ila atarudi muda sio mrefu. Unaendelea kulia na kubeba Huzuni, unakosa raha kwa muda fulani. Hiyo itabaki na wewe maisha yako yote. 



Utaitumia kama utani kuficha maumivu/lazimisha kicheko, lakini ukitulia na kutafakari unaumia na kujiuliza "sijui kwanini mama alikuwa ananiacha" (unarudi kwenye maumivu yako ktk umri ule).



Ofcoz haitakuathiri, watoto wa Kiafrika ni "tough" sio kama Wakizungu(by the path baadhi ya Watoto wa Kizungu hufanyiwa hivyo pia).


Nikukumbushe umethirika vipi na kutelekezwa/achwa na Mama yako...

1-Hujawahi kudumu kwenye Mahusino na mtu(Rafiki/Mpenzi) kwa muda mrefu kwasabu unamuhitaji kupitiliza kiasi kwamba anahisi unamnyima uhuru.


2-Mara kwa Mara unakuwa na hitaji la kuhakikishiwa kuwa Mpenzi hawezi kukuacha.

3- Unashindwa kuwa na mahusiano na mtu mmoja sababu unaogopa ukiachwa na mmoja hutokuwa na "back up".

4-Unaogopa kuwa na mahusiano ya "kudumu" aka muda mrefu aka Ndoa sababu "bora kuwa single kuliko kuachwa/telekezwa".


5-Unaamini kuwa karibu/farikiana na watu mbali mbali ni utajiri, kwamba bila kuwa karibu na watu huwezi kufika popote. Yaani huwezi kufanikisha jambo mpaka uwe karibu na watu kadhaa. 


Kidokezo: Kufahamiana na watu ni muhimu, lakini kuwa nao karibu/rafikiana nao sio muhimu.


6-Huoni shida kuacha mtoto/watoto wako na mtu mwingine kwa zaidi ya Masaa 24.


7-Ukiachwa na rafiki/Mpenzi huwa unaumia/lia sana na kwa muda mrefu. 


8-Usipojuliwa hali/rudishiwa mawasiliano na Mpenzi unaanza kuhisi kuachwa/telekezwa.



Nikirudi nitabaki hapa kwenye kuachwa/telekezwa kwenye ile "Mama yangu alikua mwema kweli, aliacha kuninyonyesha akanyonyesha mtoto wa mdogo wake" 

Usikose.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao