Skip to main content

Posts

Showing posts with the label hisia

Hebu tuone Past life yako: Kutelekezwa/Achwa...

Umekuwa na mama yako kwa Miezi 9 mpaka 11 kama ulikuwa na bahati, wengine ni miezi 6 na wengine karibu Mwaka(Miezi 12). Ni mtu pekee unaemfahamu, na unahisi kuwa upo salama na unapendwa, sababu Mtu huyu sio tu amehatarisha maisha yake ili kukubeba na kukuleta Duniani. Mtu huyu ataendelea "kuteseka" sababu unataka ule x4 usiku wa manane, ataendelea kukupenda, kukulinda, kukufunza na kukujali.  Hayo yote hutokea kwa Miezi 3 ya mwanzo, baada ya hapo unamuona mtu huyo Nusu siku, kila unapoachwa unalia sana. Siku zinavyozidi kwenda ukaribu wako na mtu huyo unapungua na kilio chako kinapungua. Kitendo cha Mtu huyo ambae sasa unamtambua kama Mama(au Anty, Dada wa Kazi ndio Mama yako) kukutelekeza/kukuacha huwa kinaumiza sana. Sasa umekua na unajitegemea kwenye mambo mengi kama vile kucheza peke yako, kujivisha viatu/nguo nk. Lakini bado ni Mtoto na bado unamuhitaji Mama yako. Jana la leo Mama amekua nyumbani siku zima, unahisi furaha, upendo na kujaaliwa.....Mama anaamua kutaka kuto

Marafiki(best) ni Milele, Wapenzi waja na kuondoka....

....kweli kabisa (kama upo chini ya miaka 29). Unapofikia umri mkubwa mambo mengi yanabadilika na unajikuta kuwa huitaji Marafiki ili kuwa na furaha(kufurahia Maisha yako). Sio hivyo tu pia unakua/badilika(nao pia) na hivyo mnakuwa hamuendani tena kama ilivyokuwa enzi zile, Matokeo yake unakuwa unafahamiana na watu na sio kurafikiana nao(best friends eeh Siwezi!). Marafiki wanakusaidia kujifunza kuhusu Maisha (kihisia), wanakusaidia kujua namna ya kukabiliana na Drama za "maisha", wanakusaidia kujua  nini cha kudharau/kushikilia Bango, wanakusaidia kujua kuwa wewe upo tofauti nao, wanakusaidia kujuana nini cha kuchangia/kutokuchangia, wanakusaidia kujua ni wakati gani unatakiwa kuachana na jambo na kusonga mbele, wanakusaidia kuelewa jambo/somo Darasani (tunauelewa tofauti) n.k. Hivyo ni Muhimu sana tena sana kwa Mtoto kutengeneza Marafiki ili aweze kujifunza hayo niliyoyataja hapo juu. Sio kila kitu Mtoto anajifunza kutoka kwa Wazazi, mengine anajifunza akiwa S