Kipajiiii....heri ya Alhamisi!
Nilipokuwa Msichana 10-17 sikuwa najali mambo ya kujiremba....Mama hakuturuhusu kupaka Rangi ya Kucha Ijumaa kisha tuondoe J'pili jioni. Eti tulikuwa tunaharibu Rangi zake...
Basi tukawa tunapaka Wino mwekundu(Pen nyekundu) au ukitaka Rangi "clear" au kucha zing'ae basi unachukua Marumaru au Vipande vya China (sahani, vikombe n.k vilivyovunjika) unasugua kwenye Sakafu ya Sementi kisha ile vumbi yake unaisugua kuchani.
Nilipofikia Miaka 18 nikaanza kupaka Wanja na Lip gloss. Nimeanza kujipangusa Poda usoni, kutinda Nyusi na kupaka Mascara nilipokuwa na miaka 28....anyways!
Baada ya kuwa addicted na Beauty Vlogger nikaamua kujitutumua kwenye kujiremba bana....basi siku ambayo najua sitoki nje mwenyewe napanga nitakavyo vyaa the next day na Vipodozi gani vya kujipaka....(Ninavyo kibao kwani kila Birthday napewa zawadi ya Vipodozi....watu wachokozi)!
Naamka mapema, nafanya shughuli zangu za ndani kisha mwanamke naketi mbele ya Kioo na kuanza kujiremba.
Mara unapigiwa simu na unatakiwa kutoka uende mahali....huyo mbio Bafuni kwenda kunawa Uso (kuondoa Vipodozi).....Jasho na Muda wote out of the window.
Najiremba ile kinachuro, ile ya kila mtu ajue kuwa nimepaka makorokocho usoni....aiii ni nipaji ambacho sikujaaliwa nacho.
Naenda kupiga Kura ya Umoja wa Ulaya...nadhani nitachagua Leba ili tubaki ndani ya Umoja huo.
Babai....
Mapendo tele kwako...
Nilipokuwa Msichana 10-17 sikuwa najali mambo ya kujiremba....Mama hakuturuhusu kupaka Rangi ya Kucha Ijumaa kisha tuondoe J'pili jioni. Eti tulikuwa tunaharibu Rangi zake...
Basi tukawa tunapaka Wino mwekundu(Pen nyekundu) au ukitaka Rangi "clear" au kucha zing'ae basi unachukua Marumaru au Vipande vya China (sahani, vikombe n.k vilivyovunjika) unasugua kwenye Sakafu ya Sementi kisha ile vumbi yake unaisugua kuchani.
Nilipofikia Miaka 18 nikaanza kupaka Wanja na Lip gloss. Nimeanza kujipangusa Poda usoni, kutinda Nyusi na kupaka Mascara nilipokuwa na miaka 28....anyways!
Baada ya kuwa addicted na Beauty Vlogger nikaamua kujitutumua kwenye kujiremba bana....basi siku ambayo najua sitoki nje mwenyewe napanga nitakavyo vyaa the next day na Vipodozi gani vya kujipaka....(Ninavyo kibao kwani kila Birthday napewa zawadi ya Vipodozi....watu wachokozi)!
Naamka mapema, nafanya shughuli zangu za ndani kisha mwanamke naketi mbele ya Kioo na kuanza kujiremba.
Mara unapigiwa simu na unatakiwa kutoka uende mahali....huyo mbio Bafuni kwenda kunawa Uso (kuondoa Vipodozi).....Jasho na Muda wote out of the window.
Najiremba ile kinachuro, ile ya kila mtu ajue kuwa nimepaka makorokocho usoni....aiii ni nipaji ambacho sikujaaliwa nacho.
Naenda kupiga Kura ya Umoja wa Ulaya...nadhani nitachagua Leba ili tubaki ndani ya Umoja huo.
Babai....
Mapendo tele kwako...
Comments