Skip to main content

Ugomvi wa Ndugu...

Sie tuliozaliwa wengi (zaidi ya wawili) huwa hatuoni umuhimu wa attention ya wazazi wetu....labda kwavile hatukupewa au tulipokuwa tukihitaji kwa vile kulikuwa na Kichanga. Tuliihsia kuambiwa "acha kudeka" na kofi juu.




Na baadhi yetu tuliishia kulea wadogo zetu ambao walihitaji attention zaidi yetu wakati Mama na Baba wako busy na mambo yao mengine kama sio kutengeneza mtoto mwingine.




Tunapenda kuwamwagia sifa kutokana na malezi yao mema kwetu na kutangaza ni namna gani tunawapenda na baadhi hudai wazazi wao ni mifano mizuri kwao (good role model)!




Wakati mwingine ni kweli ni "good role model" lakini mara nyingi ni Hatia moyoni inakufanya udhani kuwa walikuwa wazazi bora na wanafaa kuigwa....si unajua the "bila wao nisingezaliwa au kusomeshwa" sort of guilt.....




Well (1)-Uamuzi wao kukuzaa (hukuomba kuzaliwa) + (2)- ;ukumu lao kuhakikisha unaishi vizuri na unapata Elimu hivyo wacha kuhisi hatia.





Kuna mahali wazazi wetu walikosea....kwasababu kutoa "attention" ya kutosha kwa kila mtoto kati ya 3 au zaidi sio rahisi (I struggle with my 2)....!!




Watoto waliozaliwa wengi huwa wanajumuishwa linapokuja suala la "attention"....pamoja na kuwa wazazi wanaupendo wa dhati bado upungufu wa attention unaweza kusababisha matatizo ya Ukubwani.




Umewahi kujiuliza kwanini kwenye kila familia yenye watoto zaidi ya wawili (wengi) huwa kuna ugomvi kati ya siblings?!!




Inatokea Dada au Kaka anakuchukia bila sababu ya msingi.....likija suala la Mirathi ndio watu wanatoana roho kabisa....chanzo? Revisit enzi za utoto.....




Wazazi wakienda(fariki) wanaachia "hisia" zao huru....issue sio Pesa wala tamaa ni kukosea kwa wazazi wakati mkiwa wadogo.....Kuna wakati unajiuliza hivi sisi ni baba mmoja mama mmoja kweli?!!




Usichukue na kutumia maelezo haya kama ushahidi, mie sio Mtaalam nisema tu kilichonijia kichwani asubuhi ya leo....


Kuwa na Mwisho Mzuri wa Wiki.
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao