Skip to main content

Posts

Showing posts with the label asda

Maharage Mabichi kutoka Tz yauzwa ASDA-UK

Unajua ile furaha unayipata unapokula kitu kutoka kwenu ambacho hujawahi kukila ulipokuwa kwenu? Kwamba unakula kwasababu tu unahisi unampa sapoti Mkulima wa kwenu. Hii ni mara ya tatu nanunua bidhaa hii  kutoka Asda kwasababu kuu mbili. Moja ni ya kijani(sababu za kiafya na kutunza mwili) na pili ni kwasababu yanatoka Bongo. Jinsi ninavyotengeneza: (kama upo interested)... Kula na/kwa Wali kama mboga: Nayachemsha kwa sekunde kiasi kisha namimina Tui la nazi (well unga wa nazi uliochanganywa na maji ya moto). Ongezea utamu kwa mlo wako kwa kuweka Embe mbivu au Ndizi mbivu. Kula na Samaki bila Wanga: Nayachemsha  pamoja ya "maua ya coli" na "brocoli" kisha  nanyunyizia pilipili Manga na Chumvi kisha namwagia "Fish sauce" kama uonavyo picha na tuvipande twa  Samaki. Kama ni mpenzi wa Rost pia zinakwenda vema hakikisha una Gravy. Unaweza kuchanganya hizo na Kisamvu (kuungwa na Karang