Skip to main content

Posts

Miaka 20-na vs Arobaini-na kwa Mwanamke...

Heri ya mwaka Mpya! Sasa umegonga zaidi ya 40 unajisikiaje? Nakumbuka nilipokuwa in my 20s Ma-Celeb walikuwa wanasema wanajisikia kama walivyokuwa in their 20s....wakaibua msemo wa 40s in new 20s. Kwangu binanafsi nakuhakikishia sio kweli kwa asilimia Mia moja, kwasababu nilipokuwa na umri nusu wa nilionao sasa, sikuwa najiamini kwenye kufanya maamuzi Kiuchumi, Kimwili na Kimahusiano(ndugu, marafiki, mpenzi) na kijamii kwa ujumla. Kama ulichelewa kuwa na watoto basi ujue utapoteza umuhimu wa baadhi ya mahusiano na watu wengine sababu watoto wako ni muhimu zaidi kwa sasa kuliko hao watu wengine, sio hivyo tu wanao wanakupa sense ya ukamilifu na kuridhika na maisha uliyonayo na hutaki kupoteza muda kufanya mambo nje ya familia yako ulioitengeneza na Mumeo/Mkeo. Kwa wale waliokuwa na watoto ktk umri mdogo, wanaweza kuikuta wapweke sababu watoto wamekua na wanajitegemea hivyo ktk umri wa miaka 40na unaweza kujikuta unatamani kujenga mahusiano na watu wengine nje ya Mwenza wako ...
Recent posts

Ndoa ni Social construct, haina umuhimu...

....vipi kuhusu Elimu, Dini na Familia? Aah Elimu ni kwa ajili ya masikini kwani haina faida, sababu watoto wa vigogo wanainunua. But tunahitaji wajuzi wa afya ya Ubongo, Mwili na viungo vyake, Mifupa n.k kuanzia tupo tumboni mpaka tunafika miaka 120(yep tunafika huko as hii ni karne ya 21 sio 11).   Wajuzi wa mazingira,vyakula, sumu, Madawa, Nishati, Shetia na utaratibu wa kulinda na kupata Haki yako maka mtendwa au mtendewa jambo kinyume cha sheria n.k. Vipi kuhusu Imani ya Dini? Nayo tumeaminishwa tu na Wazungu na Waarabu ili watutawale si ndio? Vipi Waarabu na Wazungu huko makwao ambao bado wanafuata, kuamini na kusimamia Imani hizo za Dini, wanafanya hayo ili kujitawala? Aaah ili kunyanyasa Wanawake na watoto....Achana na Uislamu/Ukristo, vipi Imani za Dini/Miungu ya kimila na Desturi?  Bado unaamini haikuwa sehemu nzuri ya kuifanya jamii husika kuwa na structure na hivyo kufanya maisha yawe rahisi kumudu hasa linpokuja suala la stress, shida na matukio mengine ambay...

Wazazi wa Teenager leo ni...

...wale wa Miaka 30-39, isipokuwa mimi ambae naelekea miaka 50 na wanangu wala hawajafika miaka 16. Hawa teen ndio wanaoendesha Social media huku kaka/dada zao in their 20s wanasakama watoto wangu(kizazi kipya aka kizazi cha mwanzo). Nilienda kuchukua mwanangu wa Sekondari nakutana na wamama watu wazima...mie pia ni mtu mzima ila naona kama vile wenzangu wazee zaidi yangu kwa muonekano, makunyanzi na mvi...oh bila kusahau fashion. Talking about fashion, siku moja kabla ya Covid19 my Std 5 kid akanambia "kwanini unapenda kuvaa same dark colors "clothes"  nikamwambia navaa different colors but Winter coats ndio the same dull colors....halafu ikawa March 2020(deleted memories).  Anyways, turudi kwenye malezi ya watoto wenu wanaosumbua mitaa ya social media na real life. Picha kutoka comment-ini. Wengi ambao wapo in their 30s(kwa mujibu wa hiyo comment) bado ni Wanawake wa nguvu na waliamua kuwa na watoto bila Baba kwasababu wanaweza kufanya kila kitu...

Jinsi ya kulea watoto ktk Kacha mbili...

Wazazi wengi wanalea watoto wao kimagharibi bila kuishi Magharibi kwasababu Umagharibi unavutia au ni kwasababu inakufanya ujione bora, tofauti au upo juu zaidi ya wenzako ambao wanalea watoto wao kibongo-bongo ndani ya Tanzania? Usijisikie vibaya sababu hata mimi nalea wanangu kibongo-bongo wakati hawajahi kuishi Bongo kwa zaidi ya miezi kadhaa ndani ya miaka yote ya umri wao.  Humu ndani hatuwezi kutumia "kumbuka ulikotoka" au "usisahau nyumbani" sababu nyumbani kwao ni England na ndio walikotoka na walipo.... Sasa unafanyaje kuhakikisha wanao wanakuwa kibongo-bongo as well as ki-kwao(walipozaliwa)?  Picha kutoka gugo. 1: Hakikisha wanapata values na principals ulizokuwa nazo kama mbogo. Unafanikisha hili kwa kuwapa simulizi za ukweli kuyokana na uzoefu wako wa Mila na Desturi, pia kutokana na uzoefu wako wa huko mlipo na unavyoijua Kacha hiyo hakikisha una-up date inapohitajika. Mf:-  Bongo: Heshimu wakubwa wako. Ngambo: Heshimu anaekuheshimu bila kuj...