Skip to main content

Posts

Showing posts with the label kujiremba

Muendelezo wa Twiti yangu ya "if he is hot, don't let yourself go"...

Miaka mitatu iliyopita niliandika kuhusu Wanaume wapenda nachuro byuti, kama ilikupta isome hapa  kisha tuendelee. Kwanza habari za leo? mie nipo Likizo, aina ya Likizo ambapo unafanya yote uyafanyayo unapokuwa nyumbani isipokuwa haupo nyumbani. Achana na hili. Kuwa shabiki wa "natural beauty" wakati unavaa Nguo, unaoga maji Safi ya Bomba(yana Kemikali), unavuta hewa kila siku(imejaa toxic), unakula vyakula vinavyotunzwa kwa kutumia Kemikali ili kuepusha magonjwa/wadudu, Ukiugua unatumia Tiba ya Kisasa, Unatumia Simu kuwasiliana  n.k. sio rahisi. Hakuna tatizo la mtu kupenda Urembo wa Asili na hakuna tatizo kwa yeyote anaependa Urembo wa kununua/jiongezea ailimradi tu hambadilishi na kukufanya uonekane mtu mwingine. Imekuwa ni kawaida kwa baadhi ya wanaume kusakama Wanawake wanaopenda kujiremba(usually wasio kuwa na pesa, maana makeups sio chee). Kutokana na maisha yalivyo  hivi sasa (Wanawake tunafanya yaliyokuwa yakifanywa na Wanaume pekee) na mabadiliko ya Hali

Kipindi cha Baridi ndio unahisi kuwa Stylish....

Jambo! Nimeamua kuipenda Autum/Winter sasa, sio tu kuwa Kipindi hiki ndio najihisi kuwa stailishi bali pia napata nafasi ya kutumia(vaa) kila aina ya nguo niliyonayo kwa Kujiamini zaidi kwasababu hakuna  ile "presha" ya Kunyoa Kwapa wala Miguu na Mikono.....(well naficha chini ya Tights, Jaketi au Koti). Halafu Majira haya ni Marefu kuliko hizo siku 3 za Kiangazi. September Mpaka June ni total Baridi. mekosa Pic ya Mweusi ambae ana-stayle kama yangu (ubaguzi kando) Halafu pia Wivu wa hali ya hewa unakuwa hauumi sana kwa walio  Nchi za joto, unajua kuna muda unaangalia Fashinblogs za Tz halafu unapata Wivu wa hali ya hewa.....wanavalia nguo nyepesi na wanafurahia Kiangazi kwa Muda mrefu zaidi yako. Kipindi cha Kiangazi huku kinadumu kwa Mwezi mmoja, tena sio Mwezi Mzima mnapata Jua la maana bali mara mbili au tatu kwa Wiki ndani ya Miezi 3! Sasa kuna ulazima gani ya kuipenda Summer(Kiangazi)? Halafu huku tulikohamia Mwaka huu Kiangazi kilijitokeza kwa Si