Skip to main content

Posts

Showing posts with the label unyanyasaji

Rudisha Heshima Ya Ndoa: Mwenza hana Jema, kila siku Kukosoa...

Kukosoana ni jambo jema na muhimu ili kusaidia kurekebisha Tabia ndogo-ndogo ambazo ni mbaya lakini kumkosoa  Mwenza wako mara kwa mara (kupitiliza) bila wewe mwenyewe kujali kuwa unakasoro zako ambazo anazivumilia ni wazi utakuwa Mnyanyasaji. Unyanyasaji huo utamfanya mwenzio kujisikia vibaya na hivyo kusababisha:- -Maumivu ya Hisia na Akili. -Kumfanya Mwenzio ajione hana thamani au Umuhimu kwenye Ndoa yenu. -Uoga/Hofu  kwenye Ndoa yenu -Kuondoa Furaha na hivyo kujitenga kihisia -Kukosa Amani -Msongo wa Mawazo Kwasababu Mwenza wako sio Mlalamishi au Mkosoaji wa mara kwa mara haina maana kuwa wewe ni Mungu na hukosei, kwamba wewe ni next to perfect(hakuna binadamu asie na Kasoro) ndio maana Mkeo/Mumeo hajawahi kukukosoa au kulalamika. Ukweli ni kuwa, baadhi ya Weza huwa "wanakurekebisha" kwa vitendo, kwamba anafanya exactly vile unapaswa kufanya au kwa kukupa "hints" bila kuumiza Hisia zako wala kusababisha ujisikie vibaya. Asipo pata matokeo ndio ana