Skip to main content

Posts

Showing posts with the label Heshima ya Ndoa

Mama/Baba wa mtoto wa kwanza, sio wewe wa sasa!

  Unatambua kuwa ulivyo sasa kama mzazi ni tofauti na ulivyokuwa ulipoanza kuwa Mama/Baba? hasa kama watoto wako wamepishana kiasi fulani kiumri, sio tu ni kwasababu wewe na mumeo/mkeo mmkua bali pia uzoefu wenu kama wazazi unabadilika kuendana na umri wa watoto wenu. Sasa hivi unaongea na mwanao wakubwa kama watu "mzima" wenzako kwa kuwasikiliza, kuwaheshimu na wakati huo huo kuwafunza na kuwakumbusha  kuwa wao bado  ni watoto na wewe ni mzazi mwenye urafiki ila sio rafiki yao na bila kusahau kuwakumbushia uliyowafunza awali. Kwa wadogo zao ambao tuseme labda ndio toddlers, hutowalea kama ulivyowalea hao ndugu zake waliozaliwa kabla yake, kwa sababu sasa wewe ni Mjuzi wa malezi, unafanya mambo bila kuomba ushauri wala kuuliza kwa Mama au Dada au vitabu. Hakuna kinachokushangaza kwasababu yote umepitia na kwa jinsia zote mbili, unajiamini balaa. Wiki iliyopita nilipata muda wa kufikiria(surpriiiise I can actully think) jinsi nilivyobadilika tangu nilipokuwa mama kwa mara ya k

Mambo 7 Mumeo angependa umfanyie, ila...

...anaogopa kukuambia. Heri ya Mwaka mpya 2023 kwanza, leo google wamenitumia "data" bana, wanasema mwezi wa january kumekuwa na watu Laki nane na Eflu 11(8.11K) wametembelea Blog hii....nikasema Mayooo wane nimezeeka! nilikuwa napata idadi hiyo kwa Siku😅anyways, kama wewe ni mmoja wao basi nasema ahsante sana. Naendeleaje bila twita kwa Miezi 7? Vema kabisa, ahsante kwa kujali. nimegundua kuwa nina Muda mwingi sana wa kufanya mambo mengine muhimu kwa ajili ya afya ya Akili yangu. Ila baada ya kugusa miezi 4 hali ilianza kuwa ngumu nikawa nawakumbuka wote ambao tulikuwa tunabadilishana twiti mara kwa mara nikataka kushusha App, nikapata nguvu za kughaili, nikashida.  Vipi Mumeo na wanenu 3? Bado tumeshikiliana kwa mapenzi ya dhati, wanetu wanaendelea vema pia shukurani. Sema nini gharama na uhitaji wa kugawa "attention" kwa individual's umri na mahitaji yao Kiakili, Elimu, Malezi na "daily Activities" yameongezeka hyuuu!! Ila kwenye mambo mengine wan