Skip to main content

Mama/Baba wa mtoto wa kwanza, sio wewe wa sasa!

 

Unatambua kuwa ulivyo sasa kama mzazi ni tofauti na ulivyokuwa ulipoanza kuwa Mama/Baba? hasa kama watoto wako wamepishana kiasi fulani kiumri, sio tu ni kwasababu wewe na mumeo/mkeo mmkua bali pia uzoefu wenu kama wazazi unabadilika kuendana na umri wa watoto wenu.


Sasa hivi unaongea na mwanao wakubwa kama watu "mzima" wenzako kwa kuwasikiliza, kuwaheshimu na wakati huo huo kuwafunza na kuwakumbusha  kuwa wao bado  ni watoto na wewe ni mzazi mwenye urafiki ila sio rafiki yao na bila kusahau kuwakumbushia uliyowafunza awali. Kwa wadogo zao ambao tuseme labda ndio toddlers, hutowalea kama ulivyowalea hao ndugu zake waliozaliwa kabla yake, kwa sababu sasa wewe ni Mjuzi wa malezi, unafanya mambo bila kuomba ushauri wala kuuliza kwa Mama au Dada au vitabu. Hakuna kinachokushangaza kwasababu yote umepitia na kwa jinsia zote mbili, unajiamini balaa.


Wiki iliyopita nilipata muda wa kufikiria(surpriiiise I can actully think) jinsi nilivyobadilika tangu nilipokuwa mama kwa mara ya kwanza na sasa Mama kwa mara ya tatu. Namna nilianza na mwanangu wa kwanza ni tofauti kabisa na nilivyokuwa mama kwa mtoto wa pili na nilivyo sasa kwa mtoto wa tatu na wote watatu kwa pamoja.


Nikaamua kuongea na mwanagu wa kwanza kwa kuuliza swali "hey dogo unajua mama uliene sasa hivi ni tofauti kabisa na mama uliekuwa nae ulipozaliwa?" Dogo akashtuka na kuanza kuwa emotinal(alidhani namaanisha kuwa mimi sio mama yake mzazi), nikagundua nimekosea maelezo. Nikajaribu tena...."nilipokuzaa wewe nilikuwa mpya na hivyo nilikuwa makini zaidi  kwako na kwa dada yako kuliko nilivyo sasa kwa Mdogo wako.


Nikaendelea, ulipozaliwa nilikuwa nafanya kazi nje ya nyumbani hivyo nilikuwa sipati muda mwingi wa kukaa wala kucheza na wewe kwasababu nilikuwa hoi bin taabani. Halafu nilipojifungua dada yako nikabadilika tena, nikawa mama kwa watoto wawili wenye umri na jinsia tofauti, hapo nikapoteza ule-umama nilioanza nao kwako wewe mtoto wa kwanza. 


"Nikaendelea kuwa mama wa watoto wawili kwa muda mrefu, na kama mama wa nyumbani nikapata muda wa kutosha kuwalea ninavyotaka, kuwatoa nje, kucheza na nyie na kupumzika(wakilala, maana umama hauishi na hauna mapumziko). Miaka karibu nane ikapita kabla mimi na baba yako kuamua kuongeza wa 3, huyu mdogo wako nae kanibadilisha japo sio kwa kiasi kikubwa kwasababu ninyi ni wa kubwa na hivyo umakini umebaki kwenu kuliko yeye, kwa maana kuwa nime-relax zaidi(kwamba wanacheza nae na sometimes wanampa snacks na kumkataza asijiumize/haribu vitu)".


Mwanangu akasema, "aah sasa nimekuelewa mama, kwanini hukusema hivyo mwanzo badala ya kunichanganya na swali lako"? Nikamuomba msamaha. Nikakumbuka siku moja "niligombana" na wazazi kuhusu mdogo wangu ambe ni mtoto wao na walikuwa na mamlaka yote kumshauri kuhusu maamuzi ya maisha maisha  yake. Nikasema "mbona mie nilipokuwa ktk umri huo mlikuwa mnikataza kufanya anavyotaka kufanya yeye(mdogo wangu)? Wakanambia kwasababu wewe sio huyu hukuwaki(ni)cheka.


Anyways, nimekuwa Meghan Mackel kwenye Podcast yake, its all about me, me, me and more  kilakitu me. Nikutakie siku njema. Bai!

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao