Skip to main content

Posts

Showing posts with the label mazoezi

Kama Mumeo anakupenda hatoruhusu ufanye haya...

Kutokana na wakati tuliopo ambapo  kuna "informations" nyingi kuhusu nini hasa Mwanamke anapaswa kufanya au kuwa na hivyo kuibua kukanganyana na kudanganyana kuliko wakati wowote ule wa maisha ya Mwanadamu(nimeongeza chumvi, sijui historia ya Mwanamke kabla ya 1900). Hata hivyo bado haiondoi  ukweli kuwa kuwa Mwanamke  mbele ya Wanawake wa kisasa ni Kazi ya Ziada. Mara nyingi sie(wewe na wenzio) wa Kisasa huwa tunaambiana kuwa mwanaume hana haki juu ya mwili wako au uamuzi wako wa nini unataka kufanya na mwili wako(mavazi/Urembo) which it is true  kama ni Mpitaji(boyfriend) lakini ukiwa  kwenye Ndoa/Uhusiano Mwanaume kuonyesha kuwa anajali nini unaweka juu ya mwili wako ni dalili kuwa mwanaume huyo anakupenda na sio kwamba hajiamini au anahofua kuibiwa. Wengi mnadanganyana kuwa Mume(au Mume mtarajiwa) akikukataza usifanye mambo kadhaa ni kuwa anaku-control, Nyanyasa au ni Dikteta kwenye uhusiano wenu. Tunasahau kuwa yeye ni mwanaume na hivyo anajua ni namna gani Wana

Wale akina Wanangu Come First....

Hakika! wao kwanza kabla ya watu wengine baba yao included(hello Asali wa Moyo hihihihi). Hata mie nimewahi kusema/kuwaambia watu kuwa Wanangu kwanza halafu wengine na mengine ndio yanafuta. Nakumbuka nilikuwa na mwambia Mama, "nikija kuwa na mtoto, sitoruhusu mtu amshike....hata baba yake" hapo nilikuwa sijui Uchungu wa Mtoto wala Emotional connection na Bond kati ya Mimba/Mtoto na Mama. Nilihisi kuwa mtoto yupo Salama zaidi akiwa na Mama(nadhani ni Nature tu). Baada ya kuwa Mama hakika Wanangu waka wa kwanza kabla ya lolote kubwa au dogo. Maisha yangu yakazunguukwa na Wanangu na kila kitu kinachowahusu. Ikafikia mahali nikaanza kuhisi sifurahii hii "biashara" sijui "kazi" ya kuwa Mama. Ikawa too much mpaka nikasahau mimi ni nani. Nikasoma mahali (ukinipa mtihani wa Mimba, Kuzaa na kukabiliana na shida/mabadiliko ya kuwa  Mama early days baaya ya kuzaa nafaulu zaidi ya Kufaulu), maana sijawahi kusoma in my life kama nilivyosoma/ninavyoso

Come to terms with your Uchibonge....

Hello! Naweka viraka mbinguni ujue(mekuwa busy namna hiyo). Mwisho wa wiki nilipata wasaa wa kupekua pekuwa YouTube na huko nikakutana na "how to gain weight".....nikabofya na kuanza kusikiliza hadithi moja baada ya nyingine kuhusu Wanawake wanaotaka sana kunenepa. Unajua unapomsikiliza mtu au kusoma hadithi yake na kuhisi kuwa anakysemea au kukuwakilisha wewe? Yaani anakugusa kumtima. Nikakumbuka jinsi nilivyokuwa Chikonda (skinny)enzi zile nakua(nimeacha kukua nilipofikisha miaka 25 nadhani). Story Time: Nilikuwa mwembamba kiasi kwamba baadhi ya watu walidhani nina Ugonjwa. Mmoja wa Binamu zangu alikuwa akiniambia "mtu mwenyewe maiti wewe.....umebaki mifupa tu". Nilipofika late teen baadhi ya watu Familiani wakawa wanasema ninatoa mimba sana wakati sikuwa namjua mwanaume sasa sijui Mimba ziliingia kwa Roho mtakatifu! Wengine walisema naiga Uingilishi figa na hivyo kutumia madawa ya kujikondesha. Nilichoka kusakamwa kwa uchikonda wangu ambao sikuuom