Skip to main content

Wale akina Wanangu Come First....


Hakika! wao kwanza kabla ya watu wengine baba yao included(hello Asali wa Moyo hihihihi). Hata mie nimewahi kusema/kuwaambia watu kuwa Wanangu kwanza halafu wengine na mengine ndio yanafuta.




Nakumbuka nilikuwa na mwambia Mama, "nikija kuwa na mtoto, sitoruhusu mtu amshike....hata baba yake" hapo nilikuwa sijui Uchungu wa Mtoto wala Emotional connection na Bond kati ya Mimba/Mtoto na Mama. Nilihisi kuwa mtoto yupo Salama zaidi akiwa na Mama(nadhani ni Nature tu).




Baada ya kuwa Mama hakika Wanangu waka wa kwanza kabla ya lolote kubwa au dogo. Maisha yangu yakazunguukwa na Wanangu na kila kitu kinachowahusu. Ikafikia mahali nikaanza kuhisi sifurahii hii "biashara" sijui "kazi" ya kuwa Mama. Ikawa too much mpaka nikasahau mimi ni nani.




Nikasoma mahali (ukinipa mtihani wa Mimba, Kuzaa na kukabiliana na shida/mabadiliko ya kuwa  Mama early days baaya ya kuzaa nafaulu zaidi ya Kufaulu), maana sijawahi kusoma in my life kama nilivyosoma/ninavyosoma kabla ya Mimba ya Babuu mapaka leo.....bila shaka nitaendelea kusoma ili kujifunza zaidi kutokana na uzoefu wa watu wengine. Achana na hili.




Nilipomaliza kusoma nikajifunza kuwa Mama mwenye furaha anasababisha furaha ya Familia yake na hivyo watoto kukua Vema Kiakili, Kimwili, Kihisia na Ki-sosho. Sasa je utakuwaje Mama mwenye furaha?




Niliamini kuwa hakuna tatizo kwenye Uhusiano(ndoa yetu) so i was(still am) actually happy na kila kitu, isipokuwa hii "biashara" ya My kids first inaniondolea furaha kwa kuchoka Kimwili n a Kiakili, so wanangu ndio Tatizo? Hapana....Tatizo lilikuwa ni Mimi kuwaweka wao Mbele na kujisahau/kutokujua kuwa Mimi ndio Nguzo na hivyo napaswa kuwa Imara.




Mimi ndio nilitakiwa kuwa Mbele, Mimi ndio nilitakiwa kuwa wa Kwanza kabla yao ili niweze kuwaangalia na kuwatunza kwa Umakini bila kuwa na Mzigo wa Uchovu na Mawazo ya "nimepoteza Utambulisho" wangu!


Haya ndio yaliyonifanya nianze kufurahia tena Maisha kama Mama;-

1-Nalala na Kuamka Muda ule ule kila siku(kuepuka mwili kuwa comfused).


2-Naamka mapema....nusu saa kabla ya watoto na kujiandaa/pendezesha(huwa naoga Usiku tu so time saved),


3-Nafungua Madirisha


4-Watoto wanaamka Saa Moja na Nusu (sijui huwa wanaamshana hehehe)....nawaandaa wote kwa pamoja.


5-Tunafungua Kinywa Pamoja


6-By Saa 8:40am tunatoka kwenda Mdondosha Babuu Shule.

7-Narudi na kuendelea na Mipango Mingine ya Siku husika.


Nafanya Mzoezi Mara 3 kwa Wiki (Nyumbani sina pesa wala Muda wa Gym), nafanya Mazoezi Jioni kwasababu Naoga Usiku/Jioni tu. Kufanya yote hayo kwa Mpangilio huwa kunanifanya ni "look forward" kwa siku inayofuata.



Kuhitimisha: Wanangu wanakuja  baada ya Mimi. Hivyo  mimi kwanza, Watoto pili, Baba yao tatu, familia yangu(wadogo zangu na Mama).... halafu mengine na wengine hufuata.



Je wewe Mama mwenye watoto wadogo, huwa unafanya nini au unafuata mpangilio gani ili kufurahia Umama wako bila kuhisi kuwa "umepotea".....sio Dinah tena bali MamaBI au Mke wa DK(mie).


Naheshimu na Kuthamini Muda wako hapa, ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao