Skip to main content

Wale wasema "Watanzania" Wavivu/Wazembe/Waoga...


Binafsi naamini kuwa sio sahihi kumuita mtu majina ambayo unauhakika ukiitwa wewe hutofurahia iwe ni kweli upo hivyo au la! Mfano unapomuita Mwenzio Malaya unapaswa kuwa na Uhakika kuwa  Baba ni Baba yako kweli (una DNA bila rushwa).


Utamponda huyu hajitumi au Utaiponda Ofisi yake?


Sasa kwa sababu tu wewe umezaliwa au kubahatika kuwa na shughuli ya kufanya huna haki ya kuwalaumu na kuwaita majina mabaya kama vile Tegemezi, wanapenda kuomba-omba Wavivu, Wazembe, Waoga, Masikini wa Fikra n.k.



Pia wewe wa Ughaibuni, kwavile tu wewe unaishi huko ulipo na kuona Maisha ya baadhi ya "wenye Nchi" mazuri na ukapendezwa na labda utaratibu wa Serikali na kudhani Utaratibu huo umewekwa na "wananchi" hao kwa sababu sio Wavivu/Wazembe au majina yeyote machafu unayowaita Watanzania wenzako basi tambua kuwa unakosea.




Kabla ya kuanza kumlaumu na kumshutumu Mtanzania  mwenzio kuwa matizo yake yanasababishwa na yeye kuwa mvivu au kutopenda kujituma au kufanya kazi kwa bidii (wakati hakuna Kazi).....unahitaji kujua Chanzo kinachosababisha yeye kuwa hivyo unavyodhani alivyo.



Chanzo cha Matatizo ya Mtanzania au Umasikini wake na mengine yote unayomuita ni Utaratibu wa Serikali yake! sasa kama unataka kumsaidia Mtanzania huyu unapaswa kupigana ili "system" ibadilike na kusababisha mabadiliko ya "Kacha" ya Uvivu, Uzembe, Kuomba-omba n.k.



"Kacha" inatengenezwa na hivyo inaweza kubadilishwa.....kabla hujaanza kubisha unapaswa kujua Tofauti ya Utamaduni aka "Kacha" na Desturi. Desturi haibadiliki, lakini Utamaduni unaweza kubadilika kwa sababu ya Maendeleo au Mabadiliko.




Utamaduni hubadilishwa haraka kwenye Nchi husika kulazimisha Jamii kuishi kwa namna fulani, namna hiyo inaweza kuwa ya Kifukara, Kati au Juu. sasa ili Wananchi wabadilike nakuicha "kacha" ya kuomba-omba au Uvuvu ni wazi kuna Ulazima wa "system" kubadilika na kuweka sheria Mpya zinazotekerezeka.....kuondoa Mgawanyo mkubwa kati ya Masikini na tajiri.




Kwasababu Umeishi Ughaibuni na kuona  kuwa Wazungu ni watu wenye Bidii na Kujituma which is kweli kabisa lakini sio wote. Unadhani kwanini wanabidii na kujituma? Kwasababu kisheria wanapaswa kulipa Bills zao kwa wakati na wakikosa wanalipishwa "riba" sio tu kwenye Wanavyomiliki bali pia Bank inawalipisha kwa kutokuwa na pesa kwa wakati husika ambao ulijua unapaswa kulipa Bills zako.



Kuna utaratibu wa kusaidia wasio na Kazi(Benefit), Utaratibu huu ulifanya wananchi hao unaoamini kuwa wanajituma na wana bidii ya kazi (Wazungu) kuwa Wavivu nakutegemea "kukinga mikono", hii ikawa "kacha" na hivyo watu wengi wakaamua kuacha kujituma na badala yake kukaa Home na kutukana wenzao via Sosho Midia, kuangalia Tv na kucheza Games kwenye PC.



"Kacha" hiyo ikaharibu Uchumi wa Nchi kwasababu Serikali ilikuwa inatumia Pesa zaidi kuliko kuingiza  na Matokeo yake wakaamua kubadilisha utaratibu na hivyo kubana Kipato cha "Benefit" ili watu warudi Makazini.....umeona sasa?!!



Watanzania wanajituma sana tu (angalia Machinga na Mama Ntilie, Wauza Sokoni,Wlanguzi n.k), sema  Utaratibu wa Serikali yao unawaangusha. Naamini Vijana wanauweza na nguvu ya kufanya kazi na wanania ya kujituma......lakini sasa utajituma kwenye nini wakati hakuna Kazi?



Serikali ikibuni Ajira na kuweka "thamani" ya ajira kwa kuwa na kiwango cha malipo na kisheria lazima wafanya kazi walipwe hivyo au zaidi na sio chini ya Kiwango husika. Pia kuondoa "kacha" ya kila kazi kuhitaji "Kiwango cha Elimu ya Digrii kwa kazi ya Uratibu Ofisi".....Karatasi pembeni waangalie nia ya mtu na Uwezo wake wa kufanya Kazi husika(kutokana na Mahojiano), kuwe na utaratibu wa kufundisha kazi with Malipo then "Kacha" ya kusubiri kusiaidiwa au kukinga mikono, Uvivu na Uzembe itaondoka/isha.




Kama huna uwezo wa kubadilisha chanzo cha Watanzania wenzako unaowaita Wavivu/Wazembe, hawajitumi au pengine huijui Siasa wala  System ya Nchi yako hakika  kaa pembeni na uwaachie wenyewe. Bora  nisome Makala/Twiti kutoka kwa Muandishi(sio lazima awe Habari bali muandikaji mzuri na anaejua Siasa kwa mbali) kuliko kuambiwa na Celeb au Star kuwa Watanzania ni Wavivu/Hawajitumi, wanapenda kungojea wasaidiwe.




Wewe ni Celeb wa uhakika au Uchwara, una Mikataba na Projects zaidi ya tatu kwa Wiki moja, ni rahisi kwako kujituma na kufanya kazi kwa bidii kwasababu kuna "kazi" na umesaini kuzifanya na usipozifanya hakika utakosa Kipato(na mialiko itakauka) na utashtakiwa/Daiwa....sijui naeleweka!


Kwa kawaida sifanyi Siasa(siku hizi) lakini here we are! Nathamini na kuheshimu Muda wako hapa, Ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao