Skip to main content

Posts

Showing posts with the label talaka

Amina wa Ali Kiba adai Talaka Mahakamani na Kiba(2)....

Soma Mosi na Pili hapa .... Tatu, Mtoto anamuhitaji Mama yake full time kwa Miaka 5 ya mwanzo ya Maisha yake baada ya hapo PT sio mbaya. Malezi ni Kazi  kama kazi nyingine na inachosha Akili na Mwili, tofauti ni kwamba hakuna Likizo na huwezi kuacha/badilisha na pia kwa  Tz Mke (Mama wa Mtoto) huwa halipwi na hiyo inafanya kuwa "Kazi" hiyo kuonekana kuwa ni rahisi. Mkeo anapoamua au mnapokubaliana kuwa yeye abaki Nyumbani kulea watoto ni jambo zuri na la kuheshimika kwa Ulimwengu wa sasa. Mkeo akigoma kufanya Kazi ya Kulea na kuamua kwenda kufanya kazi/biashara nje ya nyumbani ni wazi kuwa mtahitaji "Mlezi" wa watoto wenu wa hapo nyumbani na yule wa "shule", na atalipwa kwa "rate" nzuri tu kulingana na Kipato/aina ya Maisha mnayoendesha. Wengi kwenye Mitandao wamelichukulia suala la Amina na Kiba kwa kuangalia Kona ya maisha waliyonayo wao kwa sasa, na sio Maisha ya Star Mkubwa mwenye Thamani ya Dollar  Millioni 5(11,570,000,000). Pi

Je! Mume huvutiwa na "u-Wife material" wa dada wa kazi?

Heri ya Mwaka Mpya! .....yanasemwa mengi juu ya Wasichana/Dada wasaidizi wa Kazi na kwanini hasa wengi huchukua "nyumba" na kuacha wenye nyumba(Wake) wakishangaa. Wengi hudhani kuwa shughuli anazozifanya Msaidizi ni shughuli ambazo Mama mwenyewe nyumba (ambae ni wife material) ndio hupaswa kuzifanya.  Sasa ikitokea Msaidizi anafanya kila kitu kuanzia kuwa "mama" mpaka Usafi wa nyumba na msimamizi wa Bajeti ya Chakula. Msaidizi huyu hana "nguvu"  ya kulalamika, kutoa changamoto au kubishana na wenye nyumba.....hasa Baba.  Msaidizi huyo siku zote huonyesha Shukurani na Heshima hata pale anapocheleweshewa Malipo(Mvumilivu). Huenda Msaidizi anafanya yote hayo kama sehemu ya Kazi yake, lakini sehemu ya Kazi yake haiji yenyewe. Kila nyumba/familia ina utaratibu wake na Mkuu wa taratibu za nyumbani huwa Mama/Mke.  Mama mwenye nyumba ndio humuelekeza Msaidizi afanye nini kwa siku husika......anamwambia afanye yale ambayo anajua Mumew