Skip to main content

Posts

Kupenda kusifiwa....

Ah! Kama wewe ni mzuri wa jambo fulani hakika utakuwa unajijua hivyo sio mbaya kujisifia mwenyewe.....au subiri Mpaka urudishe namba (ufariki) ndio watu wakusifie kwa Mema na hata kwa yale mabaya yako. Mmh! Lamini ukifariki unakuwa umemaliza ya Duniani, sasa sifa za Walimwengu uliowaacha zitakusaidia nini? Kungekuwa na uhakika wa Sifa hizo kukupunguzia Madhambi uliyofanya au Ukali wa Moto siku ya Kihama, ingekuwa Poa! Sasa, kuna Watu wameumbwa kuzitafuta Sifa kwa nguvu.....yaani mtu anatengwa, anafanyiwa maovu na mabaya yote lakini yeye yumo tu kujionyesha Mwema kwa hao Walimwengu.....wacha kujipendekeza, fanya yako....hutakiwi na huna umuhimu kwao! Unawajua wale Jamaa wanafanyiwa mabaya, wanaharibiwa familia zao au Mradi ambao ulikuwa Tegemeo kiuchumi....Jamaa waharibifu wakirudi na kuomba Msamaha wanasamehewa na Ujamaa unarudi upya. Mie siwezi bana, ukinitenda ama nalipiza Kisasi kwa Jamii yako Nzima au nakufuta akilini (nachukulia kuwa

Kuwekana...

Heloooooooo there! Mie huwa sishangai mtu akimchomekeza Jamaa yake (binamu, mtoto wa ba' mdogo).....nilishakuambia Ndugu ni wale mnaochangia Damu kwa Baba na Mama vinginevyo nyie ni jamaa tu! Hii haina "Dinah kakaa sana Ulaya kabadilika"....tangu Mdogo mie huwa siwachukulii Jamaa kuwa Ndugu! Ndugu zangu ni wale tuliotoka Tumbo Moja au Baba na Mama Mmoja.....kama hutaki kukubali bana shauri yako! Mambo ya kulazimisha Undugu bana ni kumaskishana (kutiana umasikini) na kuongezeana ma-stress tu.....hii ndio huwakosesha watu "bahati" ya kufanikiwa. Bana mie ningekuwa sijui nani ni nani Serikalini halafu kuna nafasi za kazi zinapatikana unadhani nitakuajiri wewe wakati nina Mpwa wangu (Jamaa) anaelimu na ujuzi ka' wako nyumbani? Aiii nitampa nafasi yeye kwanza, akiikataa ndio wewe wa Nje utafikiriwa. Najua sheria za kazi na kadhalika BUT Mpwa wangu sio Ndugu yangu, hatu-shei damu wala Ubini sasa undugu unatoka w

Umewahi ombwa Mchango wa Birthday?

Huu ni utovu wa nidhamu na ukosefu wa heshima wa Vipato vya watu....hii kwa Michango yote isipokuwa Ada ya Shule. Kama humudu kulisha watu kwenye sherehe ya kuadhimisha siku yako ya kuzaliwa si uachane na issue nzima ya Sherehe!! Kujitegemea Kiuchumi kumegawanyika katika makundi mbali mbali ujue...(sina uhakika, najaribu kulazimisha tu hapa hihihihihi).....! Kuna baadhi ya watu ambao huishi kutegemea wenzao ili kufanikisha mambo au jambo kwa faida zao Binafsi......wandugu jitegemeeni kiuchumi EBO!!! Mchango wa Harusi: Wakati harusi(Bikira) yenyewe wewe na mtarajiwa wako hamna hiyo HARUSI. Kama hamuwezi kulisha wageni wenu kwa kutumia vipato venu basi fungeni Ndoa mkiwa peke yenu wawili na mashahidi....eti? Siiiiiiimple + no stress. Birthday Party: hii sinimeisha isema kule juu? Eeeh kuna hii hapa chini: Michango ya Baby Shower: Kwa kawaida ukialikwa unaenda na Zawadi inayomhusu Mtoto mtarajiwa si ndio? Sasa hii biashara

Religious vs Believe in God

Nilikuambia nipo Michezoni Glasgow-Scotigo, basi bwana si nkakutana na jamaa wakaniuliza kama mimi ni Religious, nkasema hapana ila naamini Mungu.....acha washtuke!!! Udini unatutenga, Udini unasababisha watu wasifanye mambo kwa uhuru, Udini hukosesha watu wake/waume wema n.k. Hivi unajua kuwa Dini zililetwa na Wageni ambao sasa ama hawazifuati au wameamua kubadilisha waliotuaminisha kuwa "yaliandikwa" na nani sijui nani. Halafu Waafrika tunaanza kuwaona namna gani vipi hawa jamaa wanatubadilishia Maneno ya kwenye Vitabu vyetu vitakatifu ili kuendana na "maisha" ya sasa! Ama kweli Dunia imefikia mwisho. Tunajipa Moyo na kushikilia Imani zetu tukiamini kuwa ni za kweli na kuponda hao Wageni (Wamagharibi na Waarabu waliotuletea hizo Dini) kuwa ni Wafuasi wa Shetwani. Baada ya wao kuchoshwa na Imani mbili tangu Miaka 2000 iliyopita wengi wao wakaamua ama kuachana nazo au kuanzisha nyingine ili ku-suit maisha yao ya Nyakati hizi. Sasa wewe unapoteza Muda wako wote kuja