Skip to main content

Kuwekana...

Heloooooooo there!


Mie huwa sishangai mtu akimchomekeza Jamaa yake (binamu, mtoto wa ba' mdogo).....nilishakuambia Ndugu ni wale mnaochangia Damu kwa Baba na Mama vinginevyo nyie ni jamaa tu!





Hii haina "Dinah kakaa sana Ulaya kabadilika"....tangu Mdogo mie huwa siwachukulii Jamaa kuwa Ndugu! Ndugu zangu ni wale tuliotoka Tumbo Moja au Baba na Mama Mmoja.....kama hutaki kukubali bana shauri yako!





Mambo ya kulazimisha Undugu bana ni kumaskishana (kutiana umasikini) na kuongezeana ma-stress tu.....hii ndio huwakosesha watu "bahati" ya kufanikiwa.






Bana mie ningekuwa sijui nani ni nani Serikalini halafu kuna nafasi za kazi zinapatikana unadhani nitakuajiri wewe wakati nina Mpwa wangu (Jamaa) anaelimu na ujuzi ka' wako nyumbani? Aiii nitampa nafasi yeye kwanza, akiikataa ndio wewe wa Nje utafikiriwa.






Najua sheria za kazi na kadhalika BUT Mpwa wangu sio Ndugu yangu, hatu-shei damu wala Ubini sasa undugu unatoka wapi hapo?!!!




Kuwa mkweli! Hata wewe ungefanya hivyo....kila mtu anafanya hivyo.....kama hufanyi hivyo basi wewe unaroho mbaya sana.






Nakuona hapo unataka kusema "ndio maana wenzetu Wazungu wanaendelea kwasababu hawawekani"......umeishi nao? Umewahi kufanya nao kazi Nchini mwao?






Wazungu wanawekana like nothing else, tofauti ni kama nilivyosema Binamu sio Ndugu yake.....Mtoto wa Dada yako sio Ndugu yake so hata akiwaweka kwenye "Office" hakuna anaejua "connection" ya Ujamaa.




Kumuweka Mdogo wako, Mkeo au Mwanao sasa hilo ndio Kosa!


Babai.
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao