Nilijua siku nikizaa mmoja kati ya wanangu (au wote) watakuwa waongeaji sana kama errr Mimi?!!
Well, najua kuwa napenda kuongea (labda kwa vile sinywi pombe au sina nguvu ya kupigana) lakini sio muongeaji kihiiivyo.
Nakumbuka Marehemu Baba alikuwa anawaambia watu "aah kuwa makini, binti yangu huyu anamaneno sana".
Kiukweli kabisa na admit mimi ni Mbishi sana....nope! wala sina asili na watu wa Kibondo, Kigoma! Labda kwa vile sina Nguvu za kupigana lakini wakati huohuo sipendi kuonewa, sipendi kudanganywa na siamni katika "kubali yaishe" BS na wala sio "ndio bwana"....sasa nikiwa na uhakika na ninachokisema nitakubishia mpaka kesho muda kama huu.
Turudi kwenye uongeaji ambapo ndipo Babuu(my 1st born) anapokuja sasa....Laaaa! Mwanangu anaongea jamaniiiii....akianza stori zake....halafu ana "why's" za kutosha.
Maana nilikuwa nahofia Hisabati akianza shule, sasa nina shughuli ya kujibu wh