Skip to main content

Posts

Sijafa-sijaumbika....

Si nikaumwa Tetekuwanga!!! Isije siku tunakutana ukaanza kunifokea/Suta kwanini nilisema nina ngozi nzuri wakati nimejawa na madoa ka Chui(as if unajali). So wacha nijihami mapemaa. Sikutegemea kuwa siku moja ningeugua Ugonjwa huu so nilipoanza kuumwa nkasema Mimba nini? Unajua....unapofanya Mapenzi nyama kwa nyama na Mumeo kitu cha kwanza kuangalia ni Mimba kila unapojisikia vibaya ili nisijetumia Madawa nakuua au kulemaza Kiumbe(sio kwamba naitaka hiyo Mimba). Ndio hivyo sasa nimeugua gonjwa la Kiwahili(sio kweli).....akati nakua kuna watu (Majirani zetu) walikuwa wanatukuza magonjwa ya Kudumu kama vile Moyo,Kisukari nakadhalika. Utasikia "sie hatuumwi magonjwa ya Kiswahili kama Tetekuwanga, Typhod, Kifua kikuu na mengine yote ya kuambukiza. Tunaumwa Magonjwa ya maana kama vile Kisukari, Saratani, BP" hihihihihi.....sijui ulikuwa utoto wao au ujinga wao? Sitoki nje bila kujipaka tope(foundation) kuficha Madoa Meusi usoni....naaa hakuna kujiamini hapa.....natisha hahah

Chanya....Wanaume na tofauti zao (SY2)!

Hai? Baada ya sehemu ya kwanza iliyofunikwa na Hasi (bado ninazo kibawo though)nimeona sio mbaya tukiangalia zile tofauti ambazo ni Chanya. Bila kupoteza muda twendeeee! Wanakufia kimahama mpaka hawajielewi lakini sio ki-Romeo....hawa jamaa hawajui kuweka wazi hisia zao wazi kwa kukuambia wanakupenda na kukunidi na kukumisi kila siku, na Kamwe hutowasikia wakisema "bila wewe maisha yangu ni bure". Utakuwa umeambiwa/umesoma mahali kuwa Mwanaume asipokuambia hivyo ujue hakupendi.....sio kweli! Pili, wanafurahi kuonekana kama Familia, yaani siku hizi zile "date night" sijui "outings" hazipo.....kila mkitoka basi na wanenu pembeni. Ukimkumbushia "sisi"anakuambia "watoto bado wadogo kwanini tuwe wa binafsi na kujitoa wenyewe?"(family man?). Tatu, Tangu mmefunga Ndoa hakaribishi rafiki zake ambao ni Single na ukaribu wake kwao unapungua. Sio kwamba anaogopa watakuiba bali anajihisi kuwa kwenye era nyingine ya Maisha yake. Nne, Mara ya m

Baba/Mama yao Mzungu.....?

Watu(Wazungu) wanapouliza kama Mumeo/Mkeo ni Mzungu kwasababu watoto ni weusi na sio WEUSIiiiiii tii, unafurahi? Unakwazika?  au unapata (mie)nafasi ya kutoa Elimu kuwa Weusi wetu Waafrika unatofautiana na kwanini? Nilikwisha wahi gusia kuwa kuna baadhi ya watu Shuleni kwa Babuu wanadhani Baba yake ni Mzungu......nikiwa na Kibibi ambae hana rangi ng'avu sana kama Kaka yake bado watu wanadhani Baba yake ni Mzungu. Halikadhalika watoto wakiwa na Asali wa Moyo (baba yao)bado wanauliza "is their mother white"? Inafikia mahali unachoka kutoa Elimu ya tofauti ya Weusi......jamaa wanadhani Waafrika wote tuna rangi moja kwamba wote ni Chocolate au Dark Chocolate. Ikitokea unakarangi ka Caramel au umepauka zaidi basi wewe ni mixed race(toa macho kwa mshangao)! Sasa hili ni Jepesi kwa Mimi mkimama wa Kitanzania(sikwaziki kirahisi).....ilimtokea Mkimama mmoja wa USA ayeeee alikasirika mpaka akaamua kwenda public(youtube).....Weusi wa USA wapo verevere demaged na Ubaguzi. Pamoj

Kiswahili kwenye Matangazo UKtv

Sema, mambo! Kiswahili kimekuwa Common sasa kama Kiinglish, yaani inakuwa taabu kuwateta watu(not that i teta watu....). Natumia Kiswahili zaidi kuficha ukali wa maneno pale wanangu wanapoleta ujinga. Mfano tupo mtaani na watoto halafu wakawa hawasikii....unawaambia "do you want to chapwa au am going to chapa you"......wanajibu "no dont chapa us" na kuacha ujinga hehehehe. Sasa ukisema neno kuchapa kwa Lugha yao bana utaitwa abuser na unaeza nyang'anywa watoto. To the nukta: Kuna Matangazo mawili ya Kiswahili moja la Holiday (lastminutes.com) na lingine la Bank linalomhusisha Mmasai(Co-operative Bank).....nenda kaguge. Siangalii Tv kihiiiivyo ila wanangu wamenishtua niliposikia wanaimba sijui 'ninini matako'.....nkauliza "where did you learn that word?"......nikaambiwa "its only an advert mum, dont be silly". Nka-rewind si nkakutana na Tangazo la holiday jamaa anaimba kwa Kiswahili pamoja na maneno mengine akatamka "matako&