Skip to main content

Posts

Showing posts from November, 2014

Wale "naenda Africa", Natoka Africa....

Unawajua? Huwa hawasemi Nchi zao.....mf: unauliza (kwa kizungu) unatoka wapi? Wanasema "Africa"....where about in Afrika...."East Africa"....yes...where exactly? Sasa tangu Ebola ime-"cotton fire" Afrika inaitwa the Land of Ebola....hihihihihi watu hawasemi tena wanatoka Afrika bali Tanzania au nchi yeyote ambayo sio Magharibi ya Afrika (au karibu)! Kuna jamaa enzi akiwahi kusema (na wakamuamini) kuwa yeye anatoka Afrika, akaulizwa Afrika wapi....akasema "a small Country inside Tanzania called Tabata" na Baba yake ni King of Tabata! Mie siipendi Tanzania Kisiasa(sipendezwi na Siasa za Tanzania), lakini naipenda kama Nchi niliyozaliwa, na ndio maana sina (nimekataa) Ganda Jekundu kwa makusudi kabisa....(Kwa faida ya Wanangu)! Nilivyojihami hapo juu! Babai. Mapendo tele kwako...

Vyombo vya Wageni....!

Vinakaa Kwenye kabati KUUUUUUUbwa sebuleni (I used to hate that thing)....ila nilikuwa naelewa kwanini wengi wao (nilikuwa mtoto so simo) huwa na Kabati la vyombo (vitumiwavyo only wageni wakija) Sebuleni. Nyumba nyingi za kupanga ama Mna-share jiko au kila mtu anapika Sebuleni kwake kama sio nje ya mlango wake pale Koridoni/kwa nje, hivyo kuwa na Kabati la vyombo Sebuleni inaleta maana(Wapangaji sita, wote muweke makabati yenu jikoni? Hapatatosha). Achana na hilo...turudi kwenye "vyombo vya wageni"....mpaka leo (well mwaka juzi niliponunua Gold China Dinning Set and Tea Set*) ndio nimeelewa umuhimu wake. Kuwa sahihi naweza kusema nimejua umuhimu wa viatu vingi baada ya kuwa "Temp house wife", vitu kama vile kusafisha nyumba mara kadhaa kwa siku (nlikuwa nasafisha once a week, ile deep cleaning). Sasa nikienda madukani, lazima nikasalimie kwa akina "Home Departments"....yaani hadi nimeanza kuwaza mambo ya kuwa &

Kuchamba or Kutokuchamba (kwa Maji)

Wewe una prefer ipi? Kabla ya Waarabu (Wachamba kwa Maji) na Wazungu(Wachamba kwa Karatasi)....Watu walikuwa wakitumia Majani au Mchanga kujiswafi baada ya kushundi(Kutoa haja kubwa). Tulikuwa (utotoni) tunatumia "karatasi" (toilet tissues) siku maji yakikatika. Maji na Mkono ni sehemu ya "utamaduni" (ambao tuliletewa na Waarabu) na baadhi ni Usafi. Hii haina Uzungu bana, ila mambo ya kushika mavi yako moja kwa moja mie hata sipendezwi nayo!....angalau ukitumia "tissue" huyashiki mavi moja kwa moja pale mahala. Baadhi ya watu hudai kuwa wasipotumia maji hujihisi "sio wasafi" huenda ni kutokana na Mazoea au....well nenda karudie kuchamba tena kwani ni wazi umeacha mabaki. Ukitumia muda wako vizuri baada ya kushughulika utakuwa msafi(usisahau kuosha mikono kwa kutumia Sabuni hataka kama hujagusa Shundi lako). Kwanini nakuambia hivi? Well ni kwasababu ya Wanangu...najiuliza niwafunze kutu
Inapendeza sana na unapata hisia maalum za kipekee unapokutana na "High End" new publication wanazugumzia kitu ambacho wewe(Mimi) "nisiejulikana End" nimekizungumzia Mawiki na Mawiki yaliyopita! Unakumbuka Feminisim?hiyo ilikuwa Wiki iliyopita so achana nayo!....unakumbuka "kujilinganisha/fananisha"?.....aaah Dinah naona mbali sana ujue, nafaa kuwa Rais wa KissWay?!!! (*nimeacha kuchapa nacheka kwanza*). Pengine bila kujua unachapisha maelezo ya siku yako ilivyokuwa "njema" au unaweka picha au unaweza tu ku-share ulichonunua wiki hii kwa ajili ya wanao au mwenyewe n.k.....ni sehemu ya maisha yako hivyo unadhani ni poa tu uki-share na watu wanaofuatilia "kurasa" yako popote ulipo kwenye Social Media. Kuna mahali unafikia unakuwa karibu sana na watu hao ambao huwajui(mnakuwa connected), sometimes mna-miss-iana.....Jinsia tofauti hapa lazma "lust" au hata "love" hujitokeza....duh! Niliku

Zawadi kutoka kwa Mwenza!

Kwa siee wa Ulayani huwa tunapenda sana zawadi kutoka Nyumbani, zawadi (Radha ya Nyumbani) kama vile Ubuyu, Mahindi Mabichi*, Matembele ya Kukausha, Dagaa wa Kigoma, Viuongo vizima vya Pilau, Maembe Dodo au Embe Tanga bila kusahau Embe Ngong'a(unazijua?!!), Maharage ya Mbeya au yale ya Njano, Njugu Mawe n.k. Mimi binafsi huwa napata hizo mavitu moja kwa moja kutoka kwa Mama, lakini kwa wale wenye Wenza wanaopenda kwenda Bongo Mara kwa Mara huwa wanavipata moja kwa moja kutoka kwa Wenza wao. Tatizo ni kuwa Mwenza anapokuletea zawadi wakati mwingine inakuwa imetoka kwa Mme/Mke mwenzio bila wewe kujua. Inasemekana wenzetu walioungana na "rangi" tofauti huwa wana-miss sana "rangi" yao hivyo wanaporudi Nyumbani huwa rahisi kupata wanawake/wanaume ambao huwapatia kile wanachokikosa kutoka kwa wenza wao Weupe....Maisha yaha....namaanisha Haya!!! Halafu kuna wale ambao wanapenda tu kulala hovyo(Malaya)....Ujue! Ili uendelee k