Skip to main content

Kuchamba or Kutokuchamba (kwa Maji)

Wewe una prefer ipi?


Kabla ya Waarabu (Wachamba kwa Maji) na Wazungu(Wachamba kwa Karatasi)....Watu walikuwa wakitumia Majani au Mchanga kujiswafi baada ya kushundi(Kutoa haja kubwa).





Tulikuwa (utotoni) tunatumia "karatasi" (toilet tissues) siku maji yakikatika. Maji na Mkono ni sehemu ya "utamaduni" (ambao tuliletewa na Waarabu) na baadhi ni Usafi.





Hii haina Uzungu bana, ila mambo ya kushika mavi yako moja kwa moja mie hata sipendezwi nayo!....angalau ukitumia "tissue" huyashiki mavi moja kwa moja pale mahala.





Baadhi ya watu hudai kuwa wasipotumia maji hujihisi "sio wasafi" huenda ni kutokana na Mazoea au....well nenda karudie kuchamba tena kwani ni wazi umeacha mabaki.





Ukitumia muda wako vizuri baada ya kushughulika utakuwa msafi(usisahau kuosha mikono kwa kutumia Sabuni hataka kama hujagusa Shundi lako).





Kwanini nakuambia hivi? Well ni kwasababu ya Wanangu...najiuliza niwafunze kutumia Maji au niendelee na Karatasi?





Lakini kutokana na Mazingira waliopo kutumia maji itakuwa trick (sitaki kushika mavi hata kama ni ya wanangu) au a bit confusing kwao kwani kwa marafiki zao hakuna "utamaduni huo", Mashuleni haipo (unless ni shule ya Kiislamu) in which hawatokwenda.




Na-sound Mzungu sana eti?!!! Hii haina uzungu ni Logic tu.....Kutumia maji wakati unashika Mavi yako direct sio Usafi hata kama utaosha Mikono baada ya hapo!





Nakuona hapo unataka kuleta habari za "mbona Qatar kuna facilities za kuchambia bila kugusa eneo la kutolea kinyesi" au "when I was in Dubai"..... ntakutukana.





Baadhi ya Hoteli pale Dar kuna facilities za kuchambia (zina-flash mavi outta your O) but how many of us live in Hotels....eti?!!


Babai.
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao