Skip to main content

Posts

Showing posts with the label foundation

Namna ya Kuondoa Mdoa(Tetekuwanga) Usoni.....

....haraka! Najua kuwa unajua napenda ku-share kile ambacho nimejifunza na kwa sehemu kubwa ni kutokana na Uzoefu. Kwabahati mbaya niliugua Tetekuwanga(ililetwa na Schooler boy wangu). Kwasababu yeye ni Mtoto haikuwa mbaya kama mie Mtu mzima. Hii ndio nikawa naitumia Asubuhi na Usiku kama mbadala ya hiyo hapo chini Lancome Genifique ndio Serum yangu Kitambo. Mbaya zaidi Mapele yakajitokeza kwa Wingi Usoni( sijui kwanini hayakwenda Mapajani au Tumboni au Miguuni)....unapopata tatizo la Ngozi mahali ambapo sio rahisi kuficha inakupotezea Amani kabisa yaani. Hakuna Dawa ya kuondoa Mdoa hayo kwa haraka(inachukua Miezi 2 mpaka Miaka kadhaa inategemea madoa yapo deep kiasi gani Ngozini). Dactor niliandikiwa dawa ya kuondoa Madoa(mie naita Mkorogo) lakini baada ya siku chache nikahisi inaharibu ngozi yangu kwa namna nyingine, kwamba inaondoa Mdoa Meusi Usoni lakini "pores" zinapanuka/zinakuwa kubwa(sijawahi kuziona pores zangu) nikaamua kuachana nayo.

Weusi wa Ngozi sio Uchafu....

....ila usipokuwa muangalifu kwenye kuchagua Rangi za Mavazi/Nywele hakika utaonekana Mchafu(huvutii), hii  haina kujiamini.....nadhani ni muhimu kuchagua Rangi zinazoendana na Rangi ya Ngozi  yako. Mambo?!! Kuna siku nipo na mishughuliko yangu ya ndani wakati Asali wa Moyo anatazama Mashindano ya Tenesi ya Wibledoni. Anapendezwa sana na wale Williams Dadaz....mmoja wao alikuwa anacheza. Mwenyewe anafurahia uchezaji wake (au kuona Tako  kila kisketi chake kinapoinuka hihihihi maana mdada mMashallah). Sina hili wala lile nasikia mwenznagu anawasifia wadada Williams kwa kutokuwa kama Celebs wengine.....mie nkasema hao sio ma-Celeb ni Sports Stars (kwa Kiswahili ndio tunasemaje vile?) ila Media inalazimisha kuwaweka kwenye Kundi la M-aceleb kitu ambacho sio haki kwasababu wapo walipo kutokana na kazi/kujituma kwaoo na sio kuonekana kwenye Tv au kuuza Haidthi kwenye magazeti au....oh well kwa Umalaya. Katika kufunga maelezo yangu nikamalizia na....kiukweli mie siwaelewi

Ujidhaniavyo sivyo....

Heiyaaa. Mara zote huwa tunaamini tupo vile ambavyo hatupo. Nitakupa mfano:-  Unapoenda kununua Foundation(matope ya kupaka Usoni kabla ya mengineyo) unachagua rangi ambayo sio yako na huwa waaaay lighter. Sio kwamba unakusudia bali hutaki kukubali ile yako ambayo pengine inaonekana ni nyeusi sana kwenye Chupa kuliko unavyoamini(kithihitisho ni Picha zako). Enzi nilikuwa na "Wifi" wa Kiarabu na kwenye familia yao kulikuwa na waliozaliwa nje ya "uarabu" kwamba mzazi mmoja alikuwa Muarabu mwingine Mweusi halafu mtoto (binti) katokea mweusiiii mwenye nywele za kiarabu. Basi tukijikusanya tumapiga stori huyo binti alikuwa anapenda kuwasema wadada wengine kuwa ni Weusi mno kiasi kwamba hawavutii. Kwasababu mzazi wake mmoja ni Muarabu na anaishi kwenye Familia Kiarabu aliamini kuwa na yeye ni Muarabu. Hiyo pia huwatokea watoto waliochanganya na Wazungu na kuishi Uzunguni zaidi kuliko Weusini...huwa wanajidhania kuwa ni Wazungu(rangi wise). Kingine ni uwingi wa nywel