Skip to main content

Namna ya Kuondoa Mdoa(Tetekuwanga) Usoni.....


....haraka! Najua kuwa unajua napenda ku-share kile ambacho nimejifunza na kwa sehemu kubwa ni kutokana na Uzoefu. Kwabahati mbaya niliugua Tetekuwanga(ililetwa na Schooler boy wangu). Kwasababu yeye ni Mtoto haikuwa mbaya kama mie Mtu mzima.








Hii ndio nikawa naitumia Asubuhi na Usiku kama mbadala ya hiyo hapo chini

Lancome Genifique ndio Serum yangu Kitambo.


Mbaya zaidi Mapele yakajitokeza kwa Wingi Usoni( sijui kwanini hayakwenda Mapajani au Tumboni au Miguuni)....unapopata tatizo la Ngozi mahali ambapo sio rahisi kuficha inakupotezea Amani kabisa yaani.





Hakuna Dawa ya kuondoa Mdoa hayo kwa haraka(inachukua Miezi 2 mpaka Miaka kadhaa inategemea madoa yapo deep kiasi gani Ngozini). Dactor niliandikiwa dawa ya kuondoa Madoa(mie naita Mkorogo) lakini baada ya siku chache nikahisi inaharibu ngozi yangu kwa namna nyingine, kwamba inaondoa Mdoa Meusi Usoni lakini "pores" zinapanuka/zinakuwa kubwa(sijawahi kuziona pores zangu) nikaamua kuachana nayo.





Nikaamua kukubali tu kuwa naturally madoa yataondoka yenyewe, lakini sasa kutoka nje na mimadoa yangu Usoni ilikuwa inaninyima raha hivyo nikaamua kuwa navaa Matope(Foundation) kila siku. Hii ilifanya niongeze umakini wa kuitunza Ngozi yangu kwa sababu ni muhimu kuondoa "tope" usoni ili kuepusha Uharibifu wa Ngozi ambayo tayari imeharibiwa na Chickepox.





Utaratibu wangu wa kutunza Ngozi umeanza kitambo, na kama unakumbuka niliwahi kukuambia kuhusu Serum(picha ya Pili) ila sikutaka kuitaja kwasababu sikuona umuhimu wake(silipwi kutangaza) lakini leo nitakutajia kwasababu  imenisaida kwa kiasi kikubwa kuondoa Madoa Usoni.




Ila tatizo likaja kwenye Bei, Serum Genifique Mkombozi(inafanya ngozi yako kuwa Laini, kuwa sawa sawa,kuondoa mikunjo/mistari na kukupa mng'ao wa Ujana).....huo Mng'ao wa Ujana sio kwamba  niliutaka, ngozi yangu ni Mchanganyiko wa Mafuta na Ukavu hivyo nina "mng'ao asilia"  hivyo huwa naitumia Usiku tu.




Baada ya Post-Tetekuwanga si nikawa naitumia Asubuhi na Usiku, nikaona inaisha haraka, mpango wa kutumia £59 kwa Kichupa cha Seram mara Wiki kadhaa mie sina! Mkimama nikaannza kutafuta(Gugo ) Bidhaa Mbadala kutoka Kampuni Mama/Dada ya Lancome ambayo ni Loreal aiiii nikakutana na this Guy anaitwa "Youth Code" ......hapa Duniani bana kila kitu kina Mbadala wake.





Nikatumia "Kodi ya Ujana" mwaniki kwa muda wote huo well Karibu wiki Nane leo. Napenda kukuambia kuwa Wiki hii kwa mara ya Kwanza tangu June 2015 sijapaka/Vaa Tope(Foundation), Usimwambie  mtu ila "Kodi ya Ujana" inatoa matokeo yale yale ya Genifique.....jina ka' Tusi(hihihihihi) pengine better kama upo chini ya Miaka 40 lakini zaidi ya Miaka 25.




Hata hivyo Bidhaa hizi sio za kuchumbua Ngozi, isipokuwa zinaodoa rangi "ngeni" usoni....kama madoa au weusi wowote ambao sio Asilia(sio rangi yako asilia) na kufanya Ngozi yako kuwa na Rangi moja(ile uliyozaliwa nayo).


Naheshimu  na Kuthamini Muda wako hapa, Ahsante kwa kuichagua Blog hii.
Babai.

Comments

Unknown said…
bei gani na inauzwa duka la dawa au wap mm ni mhanga wa madoa ya tetekuwanga yapo kifuani blauzi za kuacha kifua wazi sivaagi plz msaada nijue bei na zinapouzwa mpnz

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao