Skip to main content

Wazungu wanajua Kupenda au wanaogopa kuonwa Wabaguzi?


Kama ulikuwa na Uzoefu mbaya na Wanaume/Wanawake wa Rangi yako hili ni Tatizo lako, na uzoefu wako mbaya haufanyi wanaume/wanawake wote wa jamii hiyo kutokujua Mapenzi/kupenda.




Linapokuja suala la kupenda kila "individual" anapenda kivyake kulingana na labda Ubora/viwango atakavyo/alivyojiwekea kutoka kwa mtu anaetaka kumpenda(well huwezi kutaka kupenda, penzi linaibukaga tu popote) na pengine ni kutaka kujaribu ili kuona wa rangi hii wapoje kama sio "attraction"(sio kila mtu anavutiwa na yeyote, wengine wanavutiwa na watu wa jamii/rangi fulani tu).






Ukiachilia mbali hayo hapo juu, pia Imani au "life situations" zinaweza kukufanya Ufunge ndoa na Mtu wa Taifa/Rangi nyingine (mostly Wazungu) ili kuboresha maisha Kiuchumi au kuapta Makazi ya Nchi fulani ambayo kutokana na Imani yako ni kuwa Utaishi maisha Bora zaidi.....au Status kama sio (hii haikuhusu wewe) kukimbia "Kacha" Maana wanawake Weusi wa Kijamaica au USA/Latino kwa DIRAMA akuuu hata mie ningeoa Mjapan(kama ningekuwa mKibaba)





Sasa unapokuwa unaishi na Mtu Mweupe kwenye Nchi ya Weupe ambapo kuna Ubaguzi dhidi ya watu wengine ambao sio Weupe, Wewe huna Uzoefu kwani umeletwa kutoka kwenye moja kati ya Nchi 54 za Afrika huko.  Mweupe wako lazima atajitahidi kutokuwa kama wenzake kwa sababu anakupenda wewe kama Mwanadamu na sio "weusi" wako.




Mweupe huyu atakuwa akiishi kwa tahadhali na kuwa makini kwa kila kitu anachokifanya au kinachofanywa na Jamii yake(Wazungu wenzake) ili usiumie. Wengine sio Wabaguzi lakini habit zao zinaweza kukufanya ujisikie kuwa unabaguliwa.





Hivyo ili kuepuka maumivu Mweupe huyu ataongeza "gestures" ambazo wewe utahisi au kudhani kuwa ni kupendwa au Mapenzi. Labda mweupe huyu anafanya mengi ili kuepuka kuonekana "mbaguzi" kwako(usijihisi Mtumwa) au Usimdhanie kuwa anaona Noma kuwa na wewe....ze puresha izi rili.





Itakuwa Ngumu kwa Mzungu wako kujadili issue zinazokugusa kwa karibu, Mfano Siasa.....utakubaliana nae au utampinga? Wengi wao wanajua kuwa Sisi Weusi ni Mabwege(well Viongozi wa Kiafrika).....ukikubaliana nae bila kumuweka sawa Utakuwa umeweka wazi Utumwa wako kwake.....Ukimpiga ni wazi malumbano yatakuwa Deeper na mwishowe utajihisi kama vile unabaguliwa.





Hebu fikiria, Mumeo/Mkeo wa Kizungu(kwa mfano) anakuambia "hebu niletee Chakula, badala ya yeye kwenda Jikoni na kujirekebishia chakula chake na Chako  na akimaliza asafishe vyombo vyote. Hakika unaenza kujihisi "Mtumwa".....lakini kama ni mweusi  hautojisikia Mtumwa wala nini, sana sana utamwambia "sema naomba"......sijui umenielewa?





Mzungu wako hawezi kukuacha ufanye kila kitu peke yako hata kama ni Mama wa nyumbani(unaangalia watoto) na yeye anafanya kazi(nje ya nyumbani), akitoka Job lazima atakusaidia kuweka watoto Kitandani n.k......hii sio kuwa anajua kupenda ila anaepuka usijione Mtumwa(in my head) hihihihihi.




Linapokuja suala la Kuneng'enuana(kuna watu wanapenda Ngono na Watumwa ujue, mambo ya kufungana kamba na kuzibana midomo, kuchapwa vibao/makofi...rafu sex eeeh.....sikuiti Mtumwa hihihihihi nachangamsha Genge  la wahuni).....Mzungu wako hapa anaweza kufanya mambo ya ajabu-ajabu wewe ukaona unapeeeeeendwa kuliko wale Weusi waliopita. Kumbe mwenzio anakuona Mtumwa....mambo yenu FANTASI.....kama hisia haziji FANTASAIZI TU.




Halafu kuna wale ambao wanapelekwa na Wazungu wao na hivyo kujikuta wanachukia kwao(wanaona aibu) wanakuwa Nazi(Ndani Weupe nje Weusi....au Kahawia?)....Anyway, nilitaka ku-blog kuhusu Mixed race kuwa "New Black", kwamba "none Mixed Black" hatuchangamki kama kizazi kipya cha " mixed race weusi" lakini nkabadili mawazo kwasababu Wasomaji wangu wengi mpo Afrika Mashariki na hamna uzoefu na kuwa "black" kwenye Nchi ya Wazungu.....so yeah!




Naheshimu Muda wako, ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao