Skip to main content

Mama wa Nyumbani kujipenda/pendeza.....Nani anakupa Ari?

Kwa sie Wafanyakazi huwa ni kawaida kushindia khanga/Pjs mwisho wa Wiki kwasababu tunatilia kila siku tuendapo kazini. Lakini je ikitokea umeamua kuwa Mama wa nyumbani kwa Muda(mie) utakuwa upo hivyo siku zote Saba za Wiki kwa Muda wote Mpaka mtoto aanze Shule?. Ni rahisi sana kujisahau na kupoteza "utambulisho" pale unapokuwa una-deal na watoto muda wote. Unafubaa, na ikiwa Nguo zako nyingi zilikuwa Office like ndio kabisaa(nani anavaa kiofisi wakati yupo nyumbani?).


Skinny Jeans nazo ni shughuli....!



Hapo ndio kutafuta Ari kunajitokeza....ni vema kuwa/kupata/kupewa Ari(kuwa Ispired that is) kwa uHasi ama uChanya.....zote ni hisia na ukizipata pengine unaweza kuzitumia kufikisha ujumbe kwa watu wengine au ukaepuka na labda kujifunza kama sio kupata nafuu kuwa "aah am  not the only one then".





Mfano: Kuna Binti mmoja Maarufu ambae Kijamii anaonekana kuwa na Mwenendo mchafu na ni Mfano mbaya kwa Mabinti wengine ambao wanakuwa "ispayadi" na mambo ya kishenzi afanyayo. Binti huyo alitajwa kuwa ni Mmoja kati ya  Wananawake wanaowapa Ari mabinti wengine. Sasa wengi(mie mmoja wapo) waliona sio sahihi kwa Mtu mwenye tabia chafu kutoa Ari kwa watu wengine(hasa wadogo).....lakini tulisahau kuwa Ari inaweza kuwa Hasi au Chanya in which zote ni muhimu(hukua unalodhani litakusaidia, mengine mwachie mwenyewe).




Mtu huwezi kumtegemea mtu mwingine(sababu tu ni Kioo cha Jamii) ajibebe utakavyo wewe ili tu wanao wasijekuharibikiwa, wanao kuharibikiwa haina uhusiano na mtu mwingine bali wewe kama Mzazi na wao wenyewe kama wao. Achana na hili!




Nakumbuka enzi natwiti kuna watu walikuwa wanakerwa na watu wanaoleta Habari za Instagram, badhi walikuwa wakisema kama umekerwa au kufurahishwa sasa si ukamalizie huko huko Insta, kwanini unatuletea sisi huku kwenye Platifomu ingine? Hawa nao hawakujua/hawajui kuwa kule ni "chanzo" kama ilivyo Twitter/Facebook kwenye Taarifa ya Habari.




Anyway, mie sio Fashionista wala Stylist na sina "style".....well nilidhani-aga Staili yangu ni "Casual chic/Smart" kumbe nlikuwa najiongopea.....hata hivyo napenda kupendeza/kuvaa vizuri lakini sifuati TRENDY. Sasa wakati wa Mimba halafu tena nikawa  STHM(stay at home mum) nikajikuta mimi na Leggings(abarikiwe aliebuni hizi makitu) tunauhusiano mzuri.





Kibibi alipoacha kunyonya na mie nikaanza kulala bila kusumbuliwa n ahivyo kuanza kufurahia Maisha(hehehehe) nkasema, nahitaji kuwa na style(ambayo bado sina), sasa natakiwa kufanya nini ili kuwa Stylish Mum of 2 in her 30s  going on 40s?(ningekuwa stylish ninge-blog)....this time nilihitaji kusikia na kuona na sio kusoma hivyo nika-Ytube.



Hakukuwa na 30s wala 40s.....wengi ni 40+(as in 50 mapaka 200? sijui),Curvy/Plus Size(hawa ni wengi hadi wanakera hihihihi fat peeps).....wakati nakaribia kukata tamaa nikakutana na Busbee Style Bonyeza hapa .  Pata Ari ili ujue wapi pa kuanzia. 


Naheshimu na kuthamini Muda wako hapa, ahsante kwa kuichagua Blogg hii

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao