Skip to main content

Posts

Showing posts with the label nywele

Kupoteza Nywele baada ya Kujifungua Update (Bidhaa)....

Natumaini Post hii itakukuta ukiwa Mzima wa afya. Kama nilivyoahidi, leo nitakuelezea utaratibu wangu uliosababisha nywele(Relaxed) zangu kurudia Afya yake baada ya kuzipoteza na kupata "upara" wa muda. Jikoni kuna mwanga asilia, sihifadhi Bidhaa hizi Jikoni....hihihi! Ukiachilia mbali kuongeza aina ya Mboga iitwayo Kale kwenye Mlo wangu wa kila siku na kula Mayai 2-3 kila asubuhi. Bidhaa hizi zimechangia kwa kiasi kikubwa kuzuia Nywele zangu kuendelea kung'oka/anguka baada ya Kujifungua. Utaratibu wangu Rahisi. Kila Siku: Napaka Cantu Shea Butter kila siku asubuhi na Jioni na baada ya kupaka Cantu huwa na-"seal" na Mafuta asilia ya Sweet Almond. Kila Wiki: Huosha na Deep Condition Nywele zangu mara Moja (kila Ijumaa/JumaMosi) na huwa natumia Cream of Nature shampoo. Baada ya hapo nafanya deep condition kwa kutumia Vitale Mayonaise ambayo huwa nachanganya na Hello hydration (haipo pichani) na aina 2 za Mafuta asilia ambayo

Kupoteza Nywele baada ya Kujifungua....update!

Ni Mwaka na Miezi kadhaa tangu nikusimulie kuhusu Nywele zangu za kichwani ambazo ni Relaxed(bila shaka). Sasa, tangu tunamaliza Mwaka nimeona sio mbaya kama niki-share safari yangu ya kuwa na Nywele  tena zenye urefu wa kutosha kutengeneza mitindo na pia zenye afya. Halafu sio mbaya kama nikikutajia/nikionyesha Bidhaa ambazo zimenisaidia kufika hapa nilipofikia. Vilevile nitakuambia ni Bidhaa gani natumia lini na kwa nini(kwenye post nyingine) na nitaambatanisha Picha. Pamoja na kusema hayo ni vema utambue kuwa Bidhaa hizi hazikuhakikishii matokeo kama yangu, inaweza kuwa bora zaidi yangu au usione mabadiliko yeyote. Baadhi ya Bidhaa hizi nilikuwa natumia kitambo, baada ya kuhangaika na kujaribu aina nyingine na kutofanikiwa nikaamua kurudi kwenye bidhaa kutoka Vitale, Nikaamua kutumia "Steamer" na "Blow dryer". Awali nilikuwa situmii Heat kabisa kama nilivyoshauriwa na Gurus. Baadae nikagundua kuwa Nywele zangu zinapenda Heat so nikarudia utaratibu w

Tulionyimwa Komwe....Faida/Hasara zake!

Tufunge na kuomba kuwa na Komwe isijekuwa Fashion kama vile kuwa na Makalio Makubwa. Tutajificha wapi? wewe utakuwa unanyoa manywele yako Usoni ili uwe na Komwe?.....well mie huwa nanyoa katikati ya Nyusi (huwa zinatishia kukutana japo sio nyingi mnaita "fuzz") pia ili kutenganisha Nyusi  na "Mstari wa Nywele" huwa na Nyoa kati kati yake! Pengine hujawahi kugundua kuwa "Hairline" yangu ipo chini hasa sehemu ya pembezoni(zoom time, usiote tu hihihihi). Umbali kutoka Nyusi kwenda kwenye Nywele ni Inchi Moja na Umbali kutoka kwenye Komwe(ambalo halipo) kwenda kwenye Nywele ni Inchi Mbili na Nusu. Kuwa na "low hairline" kuna tofautiana kama ilivyo kwenye Makomwe, tofauti hizo zinafanya baadhi kutaka kuwa na Sura ndefu na hivyo kuondoa Nywele kwa kutumia Njia mbali mbali ili nywele zisirudi(tazama Picha). Mie binafsi tayari ni ba Mdogo(sura ya kiume), sasa nikiachia Nyusi kuungana wajameni si nitasababisha mkanganyo even more(usiche