Skip to main content

Tulionyimwa Komwe....Faida/Hasara zake!


Tufunge na kuomba kuwa na Komwe isijekuwa Fashion kama vile kuwa na Makalio Makubwa. Tutajificha wapi? wewe utakuwa unanyoa manywele yako Usoni ili uwe na Komwe?.....well mie huwa nanyoa katikati ya Nyusi (huwa zinatishia kukutana japo sio nyingi mnaita "fuzz") pia ili kutenganisha Nyusi  na "Mstari wa Nywele" huwa na Nyoa kati kati yake!





Pengine hujawahi kugundua kuwa "Hairline" yangu ipo chini hasa sehemu ya pembezoni(zoom time, usiote tu hihihihi). Umbali kutoka Nyusi kwenda kwenye Nywele ni Inchi Moja na Umbali kutoka kwenye Komwe(ambalo halipo) kwenda kwenye Nywele ni Inchi Mbili na Nusu.




Kuwa na "low hairline" kuna tofautiana kama ilivyo kwenye Makomwe, tofauti hizo zinafanya baadhi kutaka kuwa na Sura ndefu na hivyo kuondoa Nywele kwa kutumia Njia mbali mbali ili nywele zisirudi(tazama Picha).




Mie binafsi tayari ni ba Mdogo(sura ya kiume), sasa nikiachia Nyusi kuungana wajameni si nitasababisha mkanganyo even more(usicheke tafadhali)? Haya twende kwenye Faida za kunyimwa Komwe:-


 -Unatumia Bidhaa za kusafisha, Kuremba na kutunza Ngozi ya Uso kwa Muda mrefu (Uso mdogo) hivyo una-save mahela.


-Hupati Chunusi kwenye Komwe ambalo huna(Paji la Uso dogo).



-Huitaji Hijabu(hahahha samahani) na ikiwa unaivaa basi inakaa vema zaidi kuliko yule mwenye Paji kuwa la Uso kubwa(Komwe).



-Paji lako la Uso linaweza kuhesabika kuwa ni "la kawaida" kwa wale wanaoweka Viwango vya Uzuri wa Mwanamke(ze Washenzi)....kuwa na Komwe sio Kawaida na kuwa na Paji dogo sana huesabika kuwa sio "kawaida" aka Ulemavu(Nenda Kaguge ili ujue lako lina Inchi ngapi)!!




-Nyusi zako huwa na afya njema kwasababu zinapata Tiba yeyote ufanyayo ili Nywele zako zinawili, Deep Condition, Oiltreatment n.k.....Nani anafanya hayo kwenye Nyusi? ni Sisi tu, tena sio kwa kutaka bali inatokea tu Automatikali.


-Unapendeza zaidi ukivaa Wigs ambazo zimenyingonya(curl).




Hasara ya kutokuwa na Komwe:-

-Kila unaposafisha Uso lazima Nywele zioshwe pia, matokeo yake unakuwa na Nywele nyepesi sehemu ya mbele kwasababu zinapitiwa na chochote unachotumia kusafisha Usoni kila siku na mara zote unaposafisha uso(unatakiwa kuosha Nywele angalau mara Moja/mbili kwa Wiki).


-Unapotibu Nywele zako kwa Mafuta na ukalala nayo, mafuta hayakawii kuteremka  Usoni na matokeo yake unapata Chunusi za ghafla.


-Kunyoa kila baada ya Wiki ili kutenganisha Nyusi na Hairline.



-Uvaa Wigs zilizonyooka(Straight) inaeza kuwa shughuli kutokelezea......unatokea kama vile Umevaa Hijabu yenye material ya "nywele".



Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao