Wiki Mpya oyee!
Nimeacha kujivunia Tanzania kama Taifa(Kisiasa) miaka kadhaa iliyopita, najivunia Tanzania kama Nchi na baadhi ya Tamaduni zake, kama vile kuvaa Vibwaya (vile vifupi, kuachia tumbo na kufunika Matiti), Ngoma na nyingine nzuri nzuri.
Kuna unataratibu wa baadhi ya wanaume kudai kuwa mwanamke yeyote atakaelala nae ni Mama yako na mtoto yeyote atakaezaliwa na mwanamke ambae sio Mama yako ni Ndugu yako. Sina uhakika kama ni Utamaduni,Tabia au pure______!
Mama yako ni yule aliekuzaa au "kisasa" aliekulea tangu ukiwa na umri wa masaa au siku chache.....sio random women aliolala nao Baba yako.
Pia ndugu yako ni yule mliotoka tumbo Moja, wengine ni Jamaa (tena ukiamua kuendeleza ujamaa huo kwani sio lazima).
Tabia ya Baba kulazimisha watoto wao kuwaita wanawake wengine Mama au watoto waliozaliwa huko (kabla au baada ya Ndoa) wadogo/kubwa zao sio haki na sio sahihi kwa mtoto/watoto husika.
Huyo ni Mkeo na hao ni watoto wako w