Skip to main content

Usinijaji....

....relax is a human nature!


Tangu u-single mother umekuwa "fashion" vijana karibu wote wa late 20s na early 30s walishazaa huko nyuma, hivyo ni ngumu kweli kukutana na mtu ambae ni "m-clean" ka' wewe (hana mtoto/watoto).




Shughuli inakuja kwa sie tuliozaa(Oa/Olewa) na Wanawake/Wanaume ambao washalizaaga "ujanani" huwa tunajajiwa sana yaani.




Unaonekana "Mwizi" kwenye jamii na familia, hata mtoto aliezaliwa kabla wewe hujakutana na Baba/Mama yake uhisi kuwa wewe ndio sababu ya Baba/Mama yake kula Buti la pua ( I know how it feels cause I was a kid once).




Unaenda mahali na Mumeo/Mkeo na tutoto twenu (bila yule wa kabla) watu wanawasonta-sonta (Shinganya Oyee!! Kusonta ni kukunyooshea kidole kama ulikuwa hujui)....anyway!




Wengine bila haya wanaanza kuuliza "nanilihu na Mama/Baba yake hawajambo" mbele yako just to piss you off....Mindugu mingine Mikosi kweli!!?




Inafikia mahali unajistukia na kuhisi kutaka kujieleza ili kuweka mambo sawa, "Ndugu jamaa na Marafiki mimi sio Mwizi, nimekutana na huyu mutu miaka 5 baadaye. Wezi ni hao walipita hapo kati kabla yangu".




Alafu unakumbuka....aiii kwani mnanisaidia kulipa Bills? Unasonga mbele kama ifuatavyo.....



Ni muhimu kuhakikisha mkibaba/Mkimama aliachana na Mkimama/Mkibaba aliezaa nae angalau miaka 2-3 kabla yako.....ili kuwe na wengine kati wamepita/pitiwa kabla yako.




*whispering* Ukiweza epuka kuoa/olewa na aliekwisha zaa kabla, unless you want to stick with an Ex for the rest of your remaining years na kujajiwa....!


I hate EXes....oh! Kumbe na mimi ni Ex wa mtu?....I hate me too.


Kwaheri kwa sasa....
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao