Skip to main content

Posts

Msingi/Malezi bora...

Habari gani? Kuna watu walikosa Malezi(Msingi) bora utotoni, malezi bora sio kula vizuri, kuvaa vizuri na kusoma shule nzuri bali kulelewa katika Mazingira ya Heshima na Adabu (kwako na kwa watu wengine), Staa/Stara, Uvumilivu, Kuridhika, Kutokata tamaa, Utu na Haiba. Hivi majuzi nimekutana na mtu akaanza nipa stori za mambo na vitu Ghali anayomfanyia Ex wake....nadhani alitaka kufikisha ujumbe kuwa yeye ni mtu wa kujali sana na kutumia Mahela kwakwe sio tatizo. Kwa bahati mbaya alikuwa hajui kuwa mimi ni Mwanamke (a bit tofauti) sibabaiki na Mahela ya watu kwani naamini ninauwezo wa kutafuta na kupata zangu.....pamoja na kusema hivyo zawadi napokea hihihihihi! Stori zikaendelea huku nami (kama kawaida) nikiuliza maswali...."Kwanini unamhudumia Ex wakati una mwanamke mpya?"...."Kuna kitu unataka au unapata kutoka kwa Ex"..."Je, Ex ana siri zako nzito unaogopa atazitoa"? n.m(na mengineyo). Kabla hatujaagana chi

Phd...

Naitaka sana yaani, sitaki kuzeeka bila kuipata....shughuli inakuja ni lini hasa nitarudi "shule"? Baada ya kupiga mahisabati nadhani by the time nagonga Miaka 50 Mwenye enzi Mungu akibariki mwanangu wa Pili (mwisho) atakuwa kwenye Teen kati hivi na huo ndio utakuwa muda mzuri. Nia sio kupanda Cheo au kugombea Uwaziri(Ubunge) la hasha! Ni kutimiza Malengo niliyojiwekea kuwa kabla sijazeeka niwe na kaelimu katika levo ya "Udaktari" Dk Dinah blablabla. Sasa angalau mie nilisomaga (si ndio nkachelewa kuzaa!Nilitaka kula life kabla ya Majukumu).....Mambo ya kutoka Binti wa_____ to Mke na Mama wa_____ in my early 20s haikunivutia....Ningeishi Mimi kama mimi lini sasa eti?!!! Anyway, kwa wale "baadhi" walioamua kuanza na Mke na Mama wa_____ hu kurudi "shule" baada ya watoto kukua which ni kitu kizuri ila unakuwa "hujayafaidi" maisha ya Usichanani....ule uhuru wa kutokuwa na Majukumu au kufikiria watoto na Mum

Pale Mwenza aongea kwa Code na rafiki zake....

Alafu mkifika nyumbani anaku-de-code-a yote....hapo sasa ama utadanganywa kabisa au utapewa robo ya ukweli(utadanganywa kwa robo tatu). Unajua upokwenda kutembelea watu mnaofahamiana au unapokuwa kwenye shughuli kwa kawaida inayojumuisha watu mbalimbali baadhi yetu tunaofahamiana/juana sana huongea kwa "Code" au unavutwa pembeni kisha unaambiwa jambo au kuombwa Msaada. Nia na madhumuni ni ili watu wengine wasielewe, wanasahau kuwa watu tunaupeo tofauti, baadhi "tunadikodi" hapo hapo......wengine ndio mpaka wasubiri "wadikodiwe" na Wenza wao watakapofika nyumbani. Natumai unaendelea vema, mimi leo bana sijielewi-elewi, yaani ka' nimepigwa au nimefanya kazi ngumu sana ningekuwa kwetu(KissWay) ningesema "nililimishwa" Usiku wa kuamkia leo. Heri ya Wiki Mpya! Babai. Mapendo tele kwako...

Ugumu wa Masomo...

Hisabati....Hisabati....Hisabati! Sikufanya Mtihani wa Mwisho kwasababu nilijua nitapata LieFu.....sikulitaka Li-F kwenye Cheti changu. Nikapiga Mahesabu ya namna ya kuepuka F kwenye Cheti changu cha Fom Foo....nikapata jibu deshi-deshi, ila mie nilitaka Deshi moja tu so siku ya Mtihani sikutokea.....nikajipatia Mathematics-!! Nilifurahiiiiiii. Nazipenda Hesabu (kuhesabu hela na Pea za viatu tu) ila kama somo hapana, sio kwamba nilikuwa siziwezi la hasha! Nilikumbuka Kanuni zote, nilifuata na kupatia njia ili kupata jibu. Tatizo lilikuja Muda napoteza muda mwingi kuhakiki jawabu matokeo yake najikuta nimefanya Maswali 5 out of 25=Efu...SIPENDI Somo la Hisabati sababu speed ya akili yangu ni a bit slow. Hakuna kitu kinachoniudhi kama kuishiwa Muda wakati wa Mtihani......Baba (Merehemu) alikuwa ananiambia "ukitaka akili yako iwe "sharp" na kuongeza uwezo wa ku-focus kwenye hesabu, fanya Mzoezi ya Hesabu mahali ambapo kuna k