Habari gani?
Kuna watu walikosa Malezi(Msingi) bora utotoni, malezi bora sio kula vizuri, kuvaa vizuri na kusoma shule nzuri bali kulelewa katika Mazingira ya Heshima na Adabu (kwako na kwa watu wengine), Staa/Stara, Uvumilivu, Kuridhika, Kutokata tamaa, Utu na Haiba.
Hivi majuzi nimekutana na mtu akaanza nipa stori za mambo na vitu Ghali anayomfanyia Ex wake....nadhani alitaka kufikisha ujumbe kuwa yeye ni mtu wa kujali sana na kutumia Mahela kwakwe sio tatizo.
Kwa bahati mbaya alikuwa hajui kuwa mimi ni Mwanamke (a bit tofauti) sibabaiki na Mahela ya watu kwani naamini ninauwezo wa kutafuta na kupata zangu.....pamoja na kusema hivyo zawadi napokea hihihihihi!
Stori zikaendelea huku nami (kama kawaida) nikiuliza maswali...."Kwanini unamhudumia Ex wakati una mwanamke mpya?"...."Kuna kitu unataka au unapata kutoka kwa Ex"..."Je, Ex ana siri zako nzito unaogopa atazitoa"? n.m(na mengineyo).
Kabla hatujaagana chini ya Ardhi ili kila mtu achukue "tube" ya huko aendako! Jamaa akanambia...."Kwani Di hujamchoka tu mumeo mpaka leo?" Nikamwambia sidhani kama kuna siku nitamchoka....akasema "well siku ikitokea basi kumbuka mie nipo".
Umeona alipotokea? Khafiri Mkubwa kabisa aliekosa malezi (Msingi) bora wa Maisha kutoka kwa Mama yake Mlezi/Mzazi.
Babai.
Mapendo tele kwako...
Kuna watu walikosa Malezi(Msingi) bora utotoni, malezi bora sio kula vizuri, kuvaa vizuri na kusoma shule nzuri bali kulelewa katika Mazingira ya Heshima na Adabu (kwako na kwa watu wengine), Staa/Stara, Uvumilivu, Kuridhika, Kutokata tamaa, Utu na Haiba.
Hivi majuzi nimekutana na mtu akaanza nipa stori za mambo na vitu Ghali anayomfanyia Ex wake....nadhani alitaka kufikisha ujumbe kuwa yeye ni mtu wa kujali sana na kutumia Mahela kwakwe sio tatizo.
Kwa bahati mbaya alikuwa hajui kuwa mimi ni Mwanamke (a bit tofauti) sibabaiki na Mahela ya watu kwani naamini ninauwezo wa kutafuta na kupata zangu.....pamoja na kusema hivyo zawadi napokea hihihihihi!
Stori zikaendelea huku nami (kama kawaida) nikiuliza maswali...."Kwanini unamhudumia Ex wakati una mwanamke mpya?"...."Kuna kitu unataka au unapata kutoka kwa Ex"..."Je, Ex ana siri zako nzito unaogopa atazitoa"? n.m(na mengineyo).
Kabla hatujaagana chini ya Ardhi ili kila mtu achukue "tube" ya huko aendako! Jamaa akanambia...."Kwani Di hujamchoka tu mumeo mpaka leo?" Nikamwambia sidhani kama kuna siku nitamchoka....akasema "well siku ikitokea basi kumbuka mie nipo".
Umeona alipotokea? Khafiri Mkubwa kabisa aliekosa malezi (Msingi) bora wa Maisha kutoka kwa Mama yake Mlezi/Mzazi.
Babai.
Mapendo tele kwako...
Comments