Skip to main content

Phd...

Naitaka sana yaani, sitaki kuzeeka bila kuipata....shughuli inakuja ni lini hasa nitarudi "shule"?



Baada ya kupiga mahisabati nadhani by the time nagonga Miaka 50 Mwenye enzi Mungu akibariki mwanangu wa Pili (mwisho) atakuwa kwenye Teen kati hivi na huo ndio utakuwa muda mzuri.




Nia sio kupanda Cheo au kugombea Uwaziri(Ubunge) la hasha! Ni kutimiza Malengo niliyojiwekea kuwa kabla sijazeeka niwe na kaelimu katika levo ya "Udaktari" Dk Dinah blablabla.




Sasa angalau mie nilisomaga (si ndio nkachelewa kuzaa!Nilitaka kula life kabla ya Majukumu).....Mambo ya kutoka Binti wa_____ to Mke na Mama wa_____ in my early 20s haikunivutia....Ningeishi Mimi kama mimi lini sasa eti?!!!




Anyway, kwa wale "baadhi" walioamua kuanza na Mke na Mama wa_____ hu kurudi "shule" baada ya watoto kukua which ni kitu kizuri ila unakuwa "hujayafaidi" maisha ya Usichanani....ule uhuru wa kutokuwa na Majukumu au kufikiria watoto na Mumeo kwenye kila maamuzi ufanyayo.




Baada ya kumaliza malezi ya watoto na kurudi "Darasani", Mwanamke (Wake) huongeza ile hali ya kujiamini kitu ambacho huwa kinawakera sana Wanaume (Waume) na kuwapotezea hali ya kujiamini.




Unakaa Darasani na Vijana eeh....(Wanaovutiwa na Wamama wenye uzoefu hihihihihihi).....Mwanamke unaaza kujisikia na kujiona bado wamo....mara Gym inaanza, Mara routine za Skin care ambazo hujawahi kuzifanya(ulikuwa busy na malezi ya watoto)....mara mavazi na ulaji vinabadilika!





Sio kwamba mwanamke unataka kutoka na Dogo-dogo la hasha! na si kweli kuwa umebadilika bali umemaliza "kulea" na huu ndio wakati wako wa kufurahia "uanamke" wako japo umegonga miaka 50na.




Sasa mie bana, nishafanya yote hayo nilipokuwa in my 20s....well ukitoa hizo routine za kujali Ngozi (nazifanya sasa).....hata nikirudi "shule" nitaendelea tu kutupia Magauni ya Khanga na Vitenge kwa heshima ya Wanangu na Baba yao na Taifa kwa ujumla!.....natania hapo kwenye Vazi.


Babai.
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao