....ambao hatuna watoto!
Kabla sijawa na Watoto sikuwahi kukwazika ikiwa mtu anazungumzia mtoto au watoto wake. Niliona ama chukulia kuwa ni sehemu muhimu ya maisha yao.
Wakati huo nilikuwa nazungumzia mambo ambayo hayahusishi "wazazi" hivyo ni wazi mimi pia nilikuwa nawakwaza wenye watoto (in my head).
Maisha tunayoishi siku hizi "Ulayani" au Ulaya ya hapa nilipo yametawaliwa na "hofu" ya ku-offend (kukwanza) wengine.....imefikia mahali mpaka Sikukuu ya Krismasi inakwaza wasiohusika (mostly Waislamu).
Yaani ule uhuru wa kuzungumza na mtu kisha kuulizia kama anawatoto haupo tena. Ila mie huwa nauliza kwanza kabla sijaanza habari za akina B-I(initials za majina ya wanagu).....wakisema hawana watoto then siwazungumzii wanangu, wakisema wanao hapo inakuwa sherehe.
Suala la watoto linatetewa kwasababu lina umiza hisia za baadhi ya watu ambao kwasababu mbalimbali hawana watoto.
Well, binafsi nimeacha k