Skip to main content

Feminism....

Na ugomvi wao wa nani ni "real Feminist", yupi ni "fake Feminist" anatumia U-feminist kama "PR" na yule sio "feminist enough". Women....WOMEN!!




Majuzi yaleee, well Wiki iliyopita)....nilipokuwa naandika post ya maJuzi yalee nikajihisi nakuwa Feminist!




Then nkakumbuka....Nimeitwa majina mengi sana mabaya, machafu na makali tangu nimeanza kujihusisha na "maisha " ya online mwaka 1999, yote huwa hayaniumi kwasababu najua mimi sio hayo majina wanayoniita (wote hawanijui zaidi ya maandishi/text).





Ila walipoanza kuniita "Dinah ni Feminist" kiasi cha kutosha, nikaanza kuchukia na kutamani kubishana au kujibu...."acha Uswahili" inakuja kichwani, nadharau na kupoteza Comments husika!





Binafsi sipendi kuitwa Feminist pamoja na kuwa baadhi ya "views" zangu za kimaisha zinaweza kukufanya udhanie kuwa mimi ni Feminist.





Sababu nyingine inayonifanya nichukie kuitwa "feminist" ni kibongo-bongo na baadhi ya Wamagharibi (stupid ones) U-Feminism unahusishwa na chuki dhidi ya wanaume au kutaka kuwa "sawa" na wanaume .





NAWAPENDA wanaume na kamwe sitaki kuwa sawa nao (isipokuwa Kiheshima, Kielimu na Kiuchumi) vingine wabaki navyo, ahsante nashukuru!.





Napenda, ninafurahia na kuridhika kusafisha nyumba yangu (sipokuwa kusafisha vyombo), kupamba na kuremba Kitanda chetu,....kupika na kumuandalia Asali wa Moyo chakula.




Napenda kuwa "in-control" kwenye masuala ya nyumbani ambayo wewe unayaita "kazi za mwanamke".....time to time Asali husaidia shughuli hizo kama wote tumekazika(wote tulikuwa job).





Oh! Kabla sijasahau...(Feminists lazima waniuwe kihisia hapa) ninaamini kuwa mwanamke anapojipendezesha halafu apite mtaani bila kupata "sifa" kutoka kwa wanaume au hata "ka mluzi", lazma atajishtukia.....Tunapendeza ili kuvutia wanaume, nao wanaume wanapendeza kutuvutia Wanawake....ni Nature!!



Babai.
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao