Skip to main content

Posts

Usafi na Kinyaa....

Ni vitu mbili tofauti....Natumai umeamka/shinda salama. Mtu kuwa msafi haina maana ana kinyaa na mwenye Kinyaa sio kwamba ni msafi pia....japokuwa wapo wasafi na wanakinyaa pia(mie).....hivi ni kinyaa au uoga wa kupata maambukizo? Nakumbuka nilipokuwa nakwenda Hospitali kwa matibabu au kumtembelea Mgonjwa....nilikuwa naumwa kichwa balaa. Nikitoka tu maeneo ya Hospitali napona. Natabia ya kubana Mkojo kwa muda mrefu(usijaribu hii ila kama ni mtu wa Kuendiketa poa) ili nisitumie vyoo vya wote(public)....Haja kubwa (sorry 4 TMI)huwa haiji nikiwa kwa watu au nje ya kwangu/kwetu.....hii sasa ni Saikoloji issue. Jana nimetoa siri yangu kwa Asali wa Moyo kuwa tukienda kwa watu(ndugu zake incl) huwa siogi wala kutumia vifaa vyao vya kujisafishia. Nitafungua Shower vema tu au kujaza Ndoo maji(inategemea nipo wapi) na kuacha shower iendelee au kumwaga maji as if naoga kumbe nanawa miguu...hihihihi. Badala ya kucheka akabaki kaduwaa hehehehehe well sina siri tena maana hata wewe msoma

Kiswahili Kigumu....spesho Post kwako!

Heyaaa. Ahsante kwa kuichagua Blog hii. Naona Idadi inaogezeka kila siku. Hi wa USA...How do you do wa hapa nilipo....jambo Afrika Mashariki.....Hello wengine wote popote mlipo Ughaibuni. Tambua kuwa ninathamini ugeni na ukazi wako wa muda mfupi au mrefu(unaposoma).....natumaini naweka makunyazi usoni kwako ama kwa kutabasamu au kwa kukunja sura. Umewahi kuamishwa(na Gugo) kutoka Kiinglishi kwenda Kiswahili halafu ukashindwa kuelewa....yaani unachanganyikiwa na hujui nini kina maanisha nini? Kwasababu ninablog kwa Kiswahili mara nyingi Gugo wananijaribu kutumia Blogger kwa Kiswahili ambayo siielewi. Mara chache nasoma Blog za Kiswahili kama vile http//www.tech255.com , www.bwaya.blogspot.com (simu haniruhusu kuweka link so yeah copy and paste uone waandikacho)na nyingine za Kuelimisha. Huko pia huwa nachanganyikiwa na kutokuelewa baadhi ya maneno ambayo nadhani ni mapya. Ila tofauti ni kuwa yapo kwenye sentensi hivyo inanirahisishia kuelewa Mwandishi alimaanisha au anamaanisha n

Vita ya Vibonge(plus size) kwenye Umodo!

Uchibonge aka Undimbo aka minyama uzembe....hello! Habari ya JumaSita? Jana nilikuwa naangalia kipindi cha Plus size War. Ambapo walizungumzia mengi kuhusiana na mwanamke kuwa mnene. Walianza na kuwasifia Bloggers wa Fashion ambao ni wanene halafu wakaenda ni nani hasa anapaswa kuwakilisha Plus sized women kwenye Umodo wa Mavazi to changamoto za wabunifu na waendesha maduka yanayouza nguo kubwa. Ila kilichonivutia zaidi ambacho nakiunga mkono kwa sababu nilikuwa najiuliza siku nyingi. Kwanini a size 14-16 anamodo kama Plus size? Well labda ni plus kwasababu UK size ndogo ya mtu mzima inayopatikana madukani ni 6 so ukiidabo au plus unapata 12 so year mie pia ni Plus size hihihihihihi. Mungu nisamehe. Binafsi nadhani Mawakala wa Plus size wanakosea.....japokiwa kwenye Documentary hii wamejielezea kwamba Soko walilonalo na demand wapatayo sio plus size tuitakayo watu wa kawaida kwamba ni size 20 to 34 au zaidi. Wanene hawana option linapokuja suala la fashion na Trend kwasababu mad

Elimisha mwanaume asibake(Rape) mwanamke....

....sio kufundisha Mwanamke jinsi ya kuzuia asibakwe! Habari ya wewe? Nasema ahsante kwa kuichagua Blog hii. Unategemea Nchi iliyoendelea kama UK kwamba huwezi kusikia suala la kuelimisha Wanaume kuhusu Ngono ili wasibake Wanawake via Media eti! Wapo wachache walioelimika na wenye kumthamini Mwanamke na kumheshimu na kutomjaji kutokana na Mavazi yake. Pia Hukumu kali dhidi ya Ubakaji inasaidia kwa mbali. Lakini bado kuna Wanawake na Wanaume ambao wanadhani kuwa Mwanamke kubakwa ni Kosa lake na hivyo kufundisha Wanawake namna ya kuzuia Kubakwa as in wasivae Mavazi yanayovutia Wanawame n.k. Mwanamke Habaki.....sasa kwanini yeye awe responsible kuji-limit kwa ajili ya Mwanaume? Kwanini Mwanaume asifunzwe kuji-control na kutomuona Mwanamke kama object ya kumalizia haja zake za Kimwili? Kanini Mwanaume asifunzwe kuwa ili kufurahia Tendo ni lazima au ni vema upande wa pili ukubali kutoa ushirikiano na sio kulazimishwa? Kwanini Mwanaume asionywe kuwa Kubaka ni Kosa? (Natambua wapo wan