Skip to main content

2014....what a Year!

Ulitegemea nitaorodhesha matukio yote ya mwaka huu? Hehehehe pole. Napenda kuwa tofauti.



Ahsante kwa kuichagua Blog hii siku ya leo ambayo ni ya Mwisho kabisa mwaka huu wa 2014, Ubarikiwe sana.





Wiki mbili zilizopita zilikuwa hectic kweli, si unajua Christmas inavyokuwa ukiwa na Watoto? Hasa mmoja ambae sasa yupo "Shule" na huko anafundishwa zaidi kuhusu "Santa na Presents" kuliko Kuzaliwa kwa Yesu...Achana na hili.






Sasa tangu nimekuwa Mama nimejikuta nasoma sana Forums zenye reviews mbalimbali kutoka kwa "real people" from Vipodozi to Kampuni za Umeme.




Nikawa kwenye Forum moja ya masuala ya Wazazi, Malezi, Mimba n.k. Nikawa nasoma review za aina ya Dawa ya Kuzuia Mimba (Uzazi wa Mpango)....mwanamke sijawahi kugusa hayo mavitu.





Kama kawaida hukosi maswali ya mabinti wadongo ambao wanataka kutumia Madawa hayo, nikisema wdogo kwa huku ninamaanisha 16 kushuka chini(inatisha, najua)!





Binti mmoja akasema anamiaka 22 na hajawahi kutumia Dawa yeyote ya kuzuia mimba zaidi ya Condoms....halafu akaomba radhi kwa kuwa "too late" kuanza kutumia Dawa hizo......hihihihihihihi nikaangalia huku na huku ili kuona kama kuna mtu ananiona(wakati nipo kwangu peke yangu).




22yrs old anajiona kachelewa kutumia Madawa ya Kuzuia mimba....mie mwenye 30na nitasemaje?





Acha uchafu, Mtu sio Mumeo, hujui hatima ya uhusiano wenu, huna mpango wa kuwa na watoto kwa sasa kwanini umruhusu akuwekee mauchafu yake mwilini mwako? Na utawekewe mara ngapi mpaka utakapofunga ndoa na kuamua kuzaa? Tumieni Condom huko mxsiii.





By the path, unataka kujua namna ya kutunza manywele yako? google "Long haire care Forum"....thank me mwakani.




Umaliziaji mzuri wa 2014, kifo hakihepukiki lakini unaweza kupunguza uwezekano....stay at home with your family.

Babai.
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao