Skip to main content

Mwanamke Kujitegemea Kiuchumi....

Ndio kukoje?


Unakumbuka enzi nipo Shule ya Msingi(just imagine...) enzi akina Taji Lihundi, Deo Mshigeni, Ramkim Ramadhani(RIP), Sunday Shomari....kabla ya akina JD hawajaja mjini....ndio walikuwa "the coolest"....Educated (well that is what I (myself) thought) watu kuwasikiliza na kuchukua "maushauri yao"....waliyokuwa wakiyasoma Ebony Magazine (sina hakika nimesema tu).

Taji Lihundi zake zilikuwa "I want a girl who can speak at lest 3 languages, independent, have a job and beautiful" by 3 languages hakumaanisha Kinyamwezi, Kihehe na Kizaramo....alitaka Malugha ya mbele huko.

Sasa huyu Baba(alikuwa mKaka then) ali-influence sana kwa akina sisi (Teenagers) enzi hizo bana, tulipofika miaka 20na na kuanza shughuli za kupenzika tukaanza kukimbia Vijana wanaoonyesha wapo sawa "kiuchumi" ili tusionekane "tegemezi".

Sasa kutokana na "muonekano" wako wa Independent....unapendeza, unavaa vitu vikali nini na nini....wanaonyesha interest wote ni wale wenye nazo....au ku-act wanazo ili wakupate, so unakuwa single, happy and Virgin kwa muda wa kutosha.

Mie sio shabiki wa Kuhongwa (japo napokea zawadi) kwasababu naamini nina uwezo na nguvu za kutafuta Pesa zangu....so babaa keep your Senti halafu ninuliage lizawadi KUU au tuunganishe tufanye jambo pamoja au nikipungukiwa niongezee.

Sijui kitu gani kinaendelea kwenye suala zima la kupeana Habari, Elimishana na kukumbushana kwenye Jamii. Napata mshituko ninaposikia siku hizi mabinti wadogo tu wanatunza wanaume, halafu wanaume wanakuwa-demanding kweli kwa wapenzi wao(wanawake) kutimiziwa mahitaji yao Kiuchumi.....tumepoteza Kizazi cha WANAUME wamebaki wanaume!

Mwanamke Kujitegemea Kiuchumi SIO kuhonga Mwanaume (unless ni Mtu mzima, upo desperate na nanilihu, aii kanunue Sanamu huko) na sio "kumtunza" mwanaume (Ni kinyume na Nature).


Hakuna kitu kinachokufanya mwanamke ujisikie umekamilika kama kuwa-looked after by mwanaume eti?!!

Pamoja na kujitegemea kwako Kiuchumi haina maana unachukua jukumu lake la kukutunza na kukuangalia wewe kama mpenzi au mkewe.

Hata Beyonce anajitegemea kiuchumi lakini Jay-Z anamtunza mkewe si eti? Well sina Mfano halisi kutoka Kioo cha Jamii Tz....so yeah!


Samahani kwa watoto na wenza wa jamaa niliowataja (ikitokea mmekatiza hapa), nyie wengine bana kama nimewakwaza just unread my Post.


Cheers!
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao