Skip to main content

Kuzaa(naturally) ni kupoteza dignity....

Heroooo!

Tangu umezaa kiasili hujahisi hali ya kujiamini zaidi kuonyesha mapaja yako(kama nguo fupi sio zako)? Au huoni big deal kuvaa vyovyote.....unaeza kwenda Sokoni na huku gagilo ljnachungulia au mkanda wa sidiria umeshuka.....pengine na night dress kabisaaaa.


Wengi husema mwanamke akizaa anapoteza hali ya kujipenda na kujijali......mie nasema sio kwamba hatujipendi na kujijali isipokuwa tumeacha DIGNITY hospitali baada ya kujichanua na kupiga makelele mbele ya watu baki ili mtoto atoke.


Halafu ukizaa nothing seem to matter but your child au children. Unapoteza ile jali ya "mimi"......maisha yako yanakuwa yamefunikwa na watu wengine ambao wanakutegemea wewe ufikirie na kufanya maamuzi kwa ajili yao.


Miezi michache ya mwanzo hali huwa mbaya sana lakini hujui wakati huo mpaka uvuke miezi 6 au mwaka hivi baada ya kujifungua hasa mtoto wa kwanza.....kwa uzoefu wangu.


Baada ya mpoto unaanza kurudi kama ulivyokuwa japokuwa dignity hairudi......Binafsi napenda kuvaa nguo fupi. Sina gauni au sketi ndefu inayovuka magotini.....ni ama gotini au juu yake au chini mpaka mwisho(well maxi).



Sasa siku Asali wa Moyo akanambia eti "Dinah wewe ni mama sasa inabidi uvae kama mama" nika hihihihihihihi halafu nikamwambia nimeshapiteza dignity wakati wa kuzaa wala sijali watu watanijajije kutokana na vijigauni vyangu.

Tunaishi kwa ajili yetu na sio kuridhisha watu wengine. Watu hawaridhiki.....utaishi wewe kama wewe lini eti.

Nikuache sasa.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao