Skip to main content

Aah namjua yule....

Hello!

Ishi ujifunze au kua uyaone.....kuna wale jamaa(wake kwa waume) huwa wana uzoefu wa kila jambo linalotokea Duniani.

Au wao wanamjua kila mhusika anaepatwa na jambo lolote interesting kwa ubaya au wema. Sijui kuhusu wewe ila mie huwa wananiudhi sana!


Unaweza ibuka unazungumzia habari ya kushtusha kuhusu mtu fulani baada ya kusikia Taarifa ya Habari then "msikilizaji wako" anaanza kukupa historia nzima ya mtu huyo na matokeo yote maishani mwake.

Unamuuliza umejuaje yote hayo mwenzangu? anakuambia "aah niliwa kuishi nae mtaa mmoja" au "mama yake alikuwa mpangaji wetu" nakadhalika!

Haiwezekani umjue kila mtu kwa undani (dont you have life?)lakini inawezekana unajua habari za kila mtu au watu wengi kwasababu ya Umbea au kwasababu unafuatilia sana habari za Kidaku.

Wakati mwingine wewe sio mbea lakini marafiki zako ni wafuatiliaji wazuri wa habari za watu na kukupa "stori".....sasa wewe kujua stori za watu haona maana kuwa unawajua sema unajua habari zao.



Sio mbaya kufuatilia Gossip hasa kwa sisi Wakimama lakini unapoleta "ufahamu" wako kuhusu mtu uliepata habari zake kwenye Magazetibya udaku usijifanye unamjua au uliwahi kuishi nae...mmsema tu umesoma.

Kwa mfano wale wenye "akili" huwa wanasema wamesoma wapi (site gani) au kitabu gani ili nawe uende ukapate Ilimi.


Si unawajua wale wenye "idea" ya mambo mengi tofauti ya Kijamii na hivyo kuyazungumzia kwa urahisi lakini kwa undani....intellectuals (hawa nawapenda) kwasababu najifunza kila wanapoleta Siasa.

Ahsante kwa kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao