Skip to main content

Posts

Kuaga au kutokuaga Marehemu!

Hiyaaaa! Leo si Halloween bana, wacha nami niungane nao kwa kuzungumzia Wafu. Jana tulikuwa (Mimi na Asali wa Moyo) tunaangalia Tv, mara Tangazo la Documentary ya Ebola (Ebola crisis) hilooo! Nkasema mie sipendi kuona/onyeshwa miili ya wafu hata kama imefunikwa(hifadhiwa vizuri), kama wameenda wameenda tu hata mkituonyesha haifanyi Ebola kuwa Hatari zaidi ya ilivyo! Mwenzangu akasema, "mie sielewi kwanini watu hupenda kwenda kutoa "Heshima" za mwisho wakitegemea kumuona Marehemu kwa mara ya Mwisho, marehemu ambae hawakuwa nae karibu kama Ndugu(wa Damu). Kwanini utake kumuona Mtu akiwa Maiti? Nikakumbuka Msiba wa Marehemu Kanumba(Mungu akuongezee heri huko uliko, Ameen), ambao sasa umekuwa (in my head) kama "model" ya Misiba ya MaCeleb wa Bongo kwa Uwingi wa watu....*whispering* nasikia MaCeleb wa Kibongo wanaombea nao wajekuzikwa na watu wengi kama huyo nliyemtaja! Walioshiriki walilalamika na wengine kukasirika kwanini hawakupewa nafasi ya "kumuona"

Wacha kuzungumzia Wanao, unatukwaza!

....ambao hatuna watoto! Kabla sijawa na Watoto sikuwahi kukwazika ikiwa mtu anazungumzia mtoto au watoto wake. Niliona ama chukulia kuwa ni sehemu muhimu ya maisha yao. Wakati huo nilikuwa nazungumzia mambo ambayo hayahusishi "wazazi" hivyo ni wazi mimi pia nilikuwa nawakwaza wenye watoto (in my head). Maisha tunayoishi siku hizi "Ulayani" au Ulaya ya hapa nilipo yametawaliwa na "hofu" ya ku-offend (kukwanza) wengine.....imefikia mahali mpaka Sikukuu ya Krismasi inakwaza wasiohusika (mostly Waislamu). Yaani ule uhuru wa kuzungumza na mtu kisha kuulizia kama anawatoto haupo tena. Ila mie huwa nauliza kwanza kabla sijaanza habari za akina B-I(initials za majina ya wanagu).....wakisema hawana watoto then siwazungumzii wanangu, wakisema wanao hapo inakuwa sherehe. Suala la watoto linatetewa kwasababu lina umiza hisia za baadhi ya watu ambao kwasababu mbalimbali hawana watoto. Well, binafsi nimeacha k

Feminism....

Na ugomvi wao wa nani ni "real Feminist", yupi ni "fake Feminist" anatumia U-feminist kama "PR" na yule sio "feminist enough". Women....WOMEN!! Majuzi yaleee, well Wiki iliyopita)....nilipokuwa naandika post ya maJuzi yalee nikajihisi nakuwa Feminist! Then nkakumbuka....Nimeitwa majina mengi sana mabaya, machafu na makali tangu nimeanza kujihusisha na "maisha " ya online mwaka 1999, yote huwa hayaniumi kwasababu najua mimi sio hayo majina wanayoniita (wote hawanijui zaidi ya maandishi/text). Ila walipoanza kuniita "Dinah ni Feminist" kiasi cha kutosha, nikaanza kuchukia na kutamani kubishana au kujibu...."acha Uswahili" inakuja kichwani, nadharau na kupoteza Comments husika! Binafsi sipendi kuitwa Feminist pamoja na kuwa baadhi ya "views" zangu za kimaisha zinaweza kukufanya udhanie kuwa mimi ni Feminist. Sababu nyingine inayonifanya nichukie kuitwa "

Vita dhidi ya Ebola imeSiasa-iwa!

Kila mtu anakuja na lake, mara Wazungu wametengeneza Ebola ili "kumaliza" Kizazi cha Weusi(Waafrika)...huyu ni Mwafrika/Mweusi aweza kuwa Manasiasa au Mtaalam(daktari) n.k. Mzungu wa kawaida (mtaani) anahoji Kwanini mnahaha na Ebola iliyoua watu Chini ya Elfu Kumi wakati Malaria inaua Mamilioni ya Waafrika kwa siku? Vipi kuhusu HIV na Umasikini ambavyo vinaondoa mamilioni ya Watu....TB je? Karibu Miezi Nane tangu mlipuko "mpya" wa Ebola kuibuka(according to my kumbukumbu) Wamagharibi walielekeza nguvu zao Ukraine na Iraqi ambako kuna faida zaidi ya kuokoa Maisha ya Muafrika, Afrika.....mara boom wanapigana zaidi kuliko wenye Tatizo (waafrika)?!! Mwenyewe jana nikajiuliza, kwanini US, EU na Cuba (is Cuba....never mind) wanapeleka "jeshi" la Wataalam kupigana na Ebola which ni more expensive kuliko kupeleke Vifaa na Wataalam wachache wa kutoa mafunzo kwa Locals (Waafrika). Nikapata jibu kuwa, labda Wazungu wanajua w