Skip to main content

Posts

Mwanao anapoleta the Ex Factor

Kwa wale ambao Uhusiano wa bf na gf uliharibika na kuvunjika kwa sababu zozote na kwa bahati mbaya mlizaa (ukizaa na mtu halafu ni X mwenzangu ni bahati mbaya). Sasa imagine kila unapowakorofisha watoto......watoto hukasirika tu hata kwa yale mema kwao.....mf unawakataza wasicheze Jikoni ni hatari au unahimiza wafanye home work badala ya kutazama Tv. Kila unapokwenda kinyume na watakavyo kama mzazi kwa faida yao wanaanza kulia au kununa na kumtaja mama au baba yao......"Baba angekuwepo ingekuwa hivi au vile" au "mama angekuwepo asingenikataza hili au lile" na hiyo huwaongezea huzuni na hata kilia kwa Uchungu bila wewe kuwaona. Mara chache unaweza kusikia wakimtaja mzazi mwenzio ambae ni mama au baba yao lakini umeachana nae na sasa unamchukia. Nimesema hayo yote kutokana na tabia ya Babuu pale unapomuudhi(ukimkataza kufanya kitu).....ananuna halafu anasema "I want my dad to come and cheer me up". Maneno hayo hunifanya nimuonee huruma (ndio atak

Nakupa mapenzi alionipa Mama....

Unless hujui Elimu ya Viumbe Hai hasa kuhusu Mwanadamu utabisha na pengine kuwa offended. Unaeza kudhani kuwa Ali Kiba amemkosea adabu Mama yake na pengine ulajiiliza utampaje mpenzi wako Mapenzi aliyokupa mama obviously hayato tosh......halafu ukawaza ni mapenzi gani hasa mwenzetu alipewa eeeh! Well uhusiano wa kwanza wa mtouo yeyote ni ule wa yeye na Wazazi wake.....mtoto hajui kupenda mtu yeyote zaidi ya wazazi wake hivyo lolote analopata kuyoka kwa wazazi hao ni mapenzi. Linapokuja penzi la mama kwa mtoto wale wa Kiume au Baba kwa Binti yake kidogo kuna mkanganyiko na wengi hushindwa kuelewa lakini kama nilivyosema ikiwa kama unalijua vema Somo la Viumbe Hai baada ya High school(ambayo mie sikuipata hii ni another sitori ya siku ingine) utaelewa. Vitendo vya kimapenzi au upendo ambavyo Mama alitupatia baada ya Kuzaliwa na kipindi tunakua ndivyo ambavyo tunavifanya au tunapenda kufanyiwa na Wapenzi wetu tukiwa watu wazima kwa......mf kunyonyana Chuchu, kukumbatiana, kupeana mab

Kuangalia na kujaji matako ya watu...!

Well sio watu wote bali Wanawake....halafu unacheka....i do! Sidhani kama ni tatizo au tabia hii inanifanya nionekane Msagaji hihiiihihi.....(ngoja nijihami kabla hujaendelea kunijaji).....hapana sina hisia na wanawake wenzangu na wala siwatamani. Nikiwa natembea kwa miguu lazima nitakuwa naangalia makalio ya yeyote aliembele yangu na kulijaji tako lake halafu kama linachekesha basi nacheka. Tena matako ya Wazungu ndio yapo ya sampuli nyingi tofauti.....ujue sisi Waafrika(well Watanzania as sijawahi nzunguuka Bara zima la Afrika)...matako yetu ni ama yapo kwamba makubwa au ya wastani na yamejitokeza au hayapo yaani bapa.....hakuna ile eneo la tako kubwaa na bapa halafu kijitako kinajitokeza kiduchu kwa chini. Au ni kwasababu Tanzania wengi hawavai Leggings sijui jeggins na viblauzi vifupi? Mmmh ukijifunga Khanga shape ya tako inaonekana so sidhani. Hao ni wanawake. Linapokuja suala la Wanaume binafsi napendezwa na wanaume ambao ni Bapa. Mambo ya kukamata tako kubwa la mumeo n

MakeUps zinaharibu Ngozi ili uzitegemee?

Biashara ya Vipodozi inapamba faya mwaka hadi mwaka asante Beauty Gurus wa Youtube.....hata mie mpaka Mascara na lipgloss nimeanza kujipaka Foundation siku hizi(well nimeanza kupaka tangu 2004). Enzi hizo mie napaka ilikuwa haiitwi Faundation bana, ilikuwa inaitwa cream to powder au mimi ndio nilikuwa sijui?hihihihihi. The thing ni kwamba most Gurus (nakojifumzia kupaka make up) ngozi zao kama vile haziko sawa. Yaani kuna mmoja siku nilivyomuona bila make up (mambo ya GRWM as in get ready with me) nilaogopa kuendelea kuangalia.....sio kwamba anatisha la hasha! Niliogopa kusikitika na kulia (tangu mekuwa mama nimekuwa way too emotional). Sasa ni mpango wa make up companies kuweka Viasili vya kuharibu Ngozi asilia ili uendelee kununua bidhaa zao na kuficha uharibifu uliopo Ngozini? Najiuliza. Au ni kutokujua kwa baadhi ya watu na hivyo walikuwa hawasafishi Ngozi na kulala na makeups? Pengine ni matumizi ya Vipodozi aka Makeup wakatu ngozi bado haijakomaa? Unajua kuwa Ngozi ni