Skip to main content

Kuangalia na kujaji matako ya watu...!

Well sio watu wote bali Wanawake....halafu unacheka....i do!


Sidhani kama ni tatizo au tabia hii inanifanya nionekane Msagaji hihiiihihi.....(ngoja nijihami kabla hujaendelea kunijaji).....hapana sina hisia na wanawake wenzangu na wala siwatamani.



Nikiwa natembea kwa miguu lazima nitakuwa naangalia makalio ya yeyote aliembele yangu na kulijaji tako lake halafu kama linachekesha basi nacheka.



Tena matako ya Wazungu ndio yapo ya sampuli nyingi tofauti.....ujue sisi Waafrika(well Watanzania as sijawahi nzunguuka Bara zima la Afrika)...matako yetu ni ama yapo kwamba makubwa au ya wastani na yamejitokeza au hayapo yaani bapa.....hakuna ile eneo la tako kubwaa na bapa halafu kijitako kinajitokeza kiduchu kwa chini.


Au ni kwasababu Tanzania wengi hawavai Leggings sijui jeggins na viblauzi vifupi? Mmmh ukijifunga Khanga shape ya tako inaonekana so sidhani.

Hao ni wanawake. Linapokuja suala la Wanaume binafsi napendezwa na wanaume ambao ni Bapa. Mambo ya kukamata tako kubwa la mumeo nani anataka bana(napenda kamata kamata).



.....tatizo linakuja kwenye Kabila langu Wanaume wengi wana ma-hips(not really) wamejazia matokeo yake si ndio na mimi nikajipatia katako ka duara hihihihihihi.


Sasa pamoja na kuwa Wanawake wa Kizungu (wa hapa nilipo) wapo kama nilivyosema hapo juu bado Wanaume wao Mashallah(as in wana mawowowo yenye shepu njema)!



Anyway.....Winter imeisha na imeniachia Cold na Mafua ya ajabu bana, nimeumwa Wiki nzima. Yaani leo ndio nimepata nguvu ya kukaa.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao