Skip to main content

Posts

Hebu tuone Past life yako: Kuachwa/Telekezwa(2)...

Jambo, ni furaha iliyoje kukutana nawe na ahsante kws kuwa nami leo. Naendelea kukumbusha Maisha uliyopitia ulipokua angali mtoto ili kuona jinsi gani yana athiri Maisha yako hasa kwenye Mahusiano na watu wengine. Kuachwa ni jambo ambalo limezoeleka sana kwenye Jamii(hata za Ulaya ya hapa), kwamba utaachwa, utalia weeee kisha utanyamaza halafu Mzazi akirudi hautokumbuka tena(asiporudi tena baada ya miezi 2? Miaka 3?). Imani hiyo hufanya Wazazi wengi kufanya maamuzi yanayo umiza mtoto(hukumbuka ila hawajui ku-express hisia zao) bila kujua(kwa sababu hata wao walifanyiwa hivyo na they turned out just fine hivyo its okay). Kuachwa/Telekezwa na Mzazi kunafananaje? Mama ambae anamnyima mtoto Nyoyo kwasababu nyingine hana tofauti na Baba ambae hajihusishi (hayupo)kwenye maisha ya mtoto.  Mzazi aliefariki wakati kabla  hujazaliwa/angali ukiwa Mdogo....athari ni zilezile. Na je ni Matendo gani yanaashiria kuwa uliachwa/telekezwa na Mama/Baba na umeathiri? 1-Unapenda "attentuon" na ku

Hebu tuone Past life yako: Kutelekezwa/Achwa...

Umekuwa na mama yako kwa Miezi 9 mpaka 11 kama ulikuwa na bahati, wengine ni miezi 6 na wengine karibu Mwaka(Miezi 12). Ni mtu pekee unaemfahamu, na unahisi kuwa upo salama na unapendwa, sababu Mtu huyu sio tu amehatarisha maisha yake ili kukubeba na kukuleta Duniani. Mtu huyu ataendelea "kuteseka" sababu unataka ule x4 usiku wa manane, ataendelea kukupenda, kukulinda, kukufunza na kukujali.  Hayo yote hutokea kwa Miezi 3 ya mwanzo, baada ya hapo unamuona mtu huyo Nusu siku, kila unapoachwa unalia sana. Siku zinavyozidi kwenda ukaribu wako na mtu huyo unapungua na kilio chako kinapungua. Kitendo cha Mtu huyo ambae sasa unamtambua kama Mama(au Anty, Dada wa Kazi ndio Mama yako) kukutelekeza/kukuacha huwa kinaumiza sana. Sasa umekua na unajitegemea kwenye mambo mengi kama vile kucheza peke yako, kujivisha viatu/nguo nk. Lakini bado ni Mtoto na bado unamuhitaji Mama yako. Jana la leo Mama amekua nyumbani siku zima, unahisi furaha, upendo na kujaaliwa.....Mama anaamua kutaka kuto

Heri kwa Mwaka 2022, hebu tuone Past life yako...

Ni kawaida kuamini kuwa ulipigwa, tishwa, telekezwa/achwa kwa masaa kadhaa au miaka na Mama/Baba na umekua vema tu, huna shida yeyote Kisaikolojia/Kimwili/Kihisia. Unaendelea kuwapenda Wazazi wako despite the mateso walikupatia ilipokuwa kichanga, Mdogo na Kijana. Unaamini kuwa walichokifanya wazazi wako ndio kimesaidia kukufanya wewe uwe hivyo ulivyo sasa. Hakika bila wazazi wako kukulea walivyokulea usingekuwa hivi ulivyo ambavyo wewe unadhani ni "kawaida". Kukubali kuwa uliteswa/na kutengwa(rejea kipengele cha kwanza) na kuwa malezo hayo yamefabya uwe ulivyo sasa lakini una kutaa kuwa huna tatizo, tayari ni tatizo.  Nikukumbushe....Kupigwa, Kutelekezwa/achwa na kutishwa kwa awamu tofauti. Kupigwa : Ikiwa Mama/Baba kukupa maumivu ya mwili ambayo uliyachukia na kuogopa kwanini unatumia mbinu hiyo hiyo kuumiza mtoto wako? Mtoto anapofanya kosa(bado anajifunza), kwanini huchukui hatua na kumfunza/elewesha na kisha kumpa adhabu kulingana na umli wake ambayo sio kipigo.  Kwanini

Kujali(nguzo 5 za Mahusiano.

 Huwezi kuwa Mke bora ikiwa hufanyi mambo Milioni moja na nusu ikiwa ni pamoja na Kujali.  Kujali kwenye Ndoa  sio kitu kinachotakiwa kufanywa na Mke, bali Mume pia. Japokuwa  kwenye jamii Mke ndio hutegemewa kuonyesha kujali zaidi kuliko mwenza wake wa kiume. Mke atahakikisha Mume analala mahali safi na comfortable, nyumba safi na inapendeza, Nguo na hata Chakula kimeandaliwa vema na kwa wakati. Mke hatoishia hapo, atajiswafi na kujiremba/pendezesha/nukia vizuri kwa ajili ya Macho na Heshima kwa Mume(watu watakao kuona nje). Mke ataendelea kutoa ushari, kumtuliza, kumpa moyo/matumaini, kum-support, kuhakikisha ana Afya njema na kumkumbusha suala zima la kuilinda Afya yake. Ikiwa mnaishi mbali na Wazazi wa Mume, Mke atakumbusha kuwajulia hali na pengine kwenda kama Familia ili wasipoteze ukaribu kwako na Wajukuu zao. Mwisho kabisa, Mke atahakikisha watoto wanakubuka siku Muhimu kwa Baba yao na kukupatia vijizawadi kwa niaba yao(Watoto)   Uliza Mumeo anakujali kwa  kufanya nini? Kwa 99%