Skip to main content

Mzazi Mkali Vs Mpole....


Hello!

Utakoma na Post za Wazazi na Watoto mahali hapa, ni maisha niishiyo sasa na sio mbaya kama nikichangia uzoefu wangu ambao pengine unafanana na wako na hivyo kukufanya kujisikia nafuu kuwa haupo peke yako au ukanishangaa. Vilevile inawezekana kabisa ukajifunza jambo!




Hofu yangu kuu ni Waanangu kuwa na Tabia mbaya chini ya uangalizi wangu, kutokuwa na Heshima kwetu Wazazi wao na Watu wengine. Hofu hii ndio iliyochangia mimi kujitolea Mhanga na kuwa Mama wa nyumbani kwa Miaka 3.  Sikutaka Wanangu waje na tabia za "Nursery assistant".....Babuu alianza Nursery akiwa Mchanga as bado nilikuwa na ile " I can do all, independent woman".....untill Mwanangu alipoanza kunikataa na kulia kwa Uchungu kila nilipokuwa naenda kumchukua!




Vilevile alipofikisha Miezi 8 akawa na "vijitabia" ambavyo siku pendezwa navyo.....Solution? nikapunguza Masaa ya Kazi na Nursery(so kutoka full time akawa anaenda kwa 5hrs). Niliamini(bado naamini) kuwa Mtoto anahitaji Mama yake  24/5 (ondoa  Masaa ya Nursery) Miaka 5 ya mwanzo ya Maisha yake(mie sio Feminist so nisamehe kama sitomtaja sana Baba).




Kiasilia Mimi ni Mkali(sipendi ujinga), inawezekana ni kwasababu ya kuwa na wadogo wengi zaidi kuliko kuwa na wakubwa(mie ni wa Pili kuzaliwa na ni Dada mkubwa). Ukali wangu ni kwa watoto wote sio wadogo zangu tu(walipokuwa wadogo) bali hata kwa watoto wa Watu niliokua na "babysit" au wale waliokuwa wakija kunitembelea kutokana na kufahamianakwangu na Wazazi wao.




Pamoja na Ukali pia mimi ni Manners "fanatic"(usiende kuGugo), nachukia watu/watoto wasio na Manners. Mara zote huwa napitisha Hukumu kuwa Mama zao hawakuwafunza, kwasababu naamini mtoto anajifunza "manners" kati ya Miaka 2 na 5, uki-"lemaa" katika Umri huo basi wewe na wao are done!



Kuanza kumfunza mtoto Manners katika Umri mkubwa ni kazi zaidi kuliko umri nilioutaja hapo juu, umri wa Miaka 2-5 mtoto hujifunnza "misingi" ya mambo mengi na kuitunza, hivyo ukianza  mapema inakuwa rahisi "kumkumbushia" akivuka umri huo kuliko kuanza upya.




Kumbuka mtoto anapozaliwa huwa hajui kitu(well labda kunyonya), Ubongo wake huwa "pure", sasa yote mfanyayo kama wazazi au Mlezi(kwa wale wanaoachia watoto watu wengine) huwa ni mara ya Kwanza kwa Mtoto. Mungu anisaidie na kunipa nguvu ili Wanangu wakue wakijua umuhimu wa kuwa Wema, kuheshimu, kuomba na kushukuru.




Kwenye Familia yetu ya watu Wanne, Mimi Mama ni Mkali/Mnoko) na Baba yao ni Mpole(laid back)....kuna mahali tulikuwa tunapishana kwenye malezi, kwamba mimi nikikataza Watoto wasifanye jambo, wanakimbilia kwa Asali wa Moyo(baba yao) na yeye anawakubalia. Ikafikia Dad akawa their best friend na mie nikawa sio Friend of any sort hihihihi.



Ikabidi "Work as a Team" iingizwe ili Watoto wajue kuwa Mama akisema HAPANA basi hata wakikimbilia kwa Baba ni HAPANA. Haikuwa rahisi kama kwenye  kila kitu  unachowafunza kwenye Umri huo mdogo.


Pamoja na ukali wangu, sijawahi kuwachapa, vitisho kama "I will call Nunda for you", "will give you Time out", will taka away Toys au Tablets bado zinafanya kazi. Sasa wewe ni Mzazi wa aina gani/ Mkali/Mnoko au Mpole?


**Nunda= to them is like a Monster


Ahsante kwa Muda wako hapa, nathamini na kuheshimu uamuzi wako wa Kuichagua Blog hii.

Babai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao