Skip to main content

Enzi tulitongozwa uchochoroni...

Miaka 10 iliyopita mlitongozana kwa texts au kwa sauti baada ya kuona picha, nasikia siku hizi wala hamtongozwi kabisa au nyie ndio mmekuwa watongozaji. Wanawake wamekua wawindaji, watafutaji, wapiganaji....wanaume wanafanya nini? 



Basi sie "Mid Gen X" a.k.a Xennials a.k.a MillenX (tulizaliwa 1975-85) tulikuwa tunakimbiliwa huku tunaitwa " oyaa mrembo" au "oyaa dada'ke (weka jina la kaka yako)" au hey Binti (weka jina la Baba yako), kama jamaa humtaki/hakuvutii unakimbia kama athletes au unaingia kwenye nyumba yeyote unatulia mpaka jamaa apitilize au ageuze na kurudi kijiweni, then unaendelea na safari zako au inatokea mtu kwenye nyumba hiyo anakisindikiza so unakuwa pretected. Kama jamaa unamkubali basi unapunguza mwendo so anakufikia haraka. 



Mnatembea huku anakuuliza maswali kisha mnafika kichochoroni(hakuna watu wengi) then anashusha mistari yake...unadengua-dengua pale na kujiringisha(hiba ya kike) huku unachora chini au unatafuna kucha...unamuangalia machoni, unaona aibu kisha unageuka upande mwingine unamuambia "nipe muda nifikirie" au "subiri  nitakupa jibu"....anaanza kukubembeleza umkubali hapo hapo ili roho yake itulie....unang'aka...anakuomba radhi. Anauliza sasa lini utampa jibu...unamwambia labda wiki Ijayo...jamaa anaona ni mbali ila ndio inabidi aheshimu. Anakuaga na kukuuliza kama unataka akusindikize? Gentleman wa Kiswahili(as in culture not life style).



Mnaachana, anakupa tabasamu mwanana. Sasa presha inaanza ya kutoa jibu...unawaza mambo kibao ya sasa, shule, unoko wa wazazi na maisha yenu ya baadae....unajiuliza vipi kama hana kazi na tukapaya HIV?  na ukashika mimba, je ataweza kunitunza mimi na mtoto wetu? 

                                              Jamaa anaomba jibu lake na wewe huna moango nae.


Baada ya kufika nyumbani unahisi baba na mama yako wanajua  yaliyoujaza Moyo na akili yako, unajitahidi ku-act normal kumbe unakosea na wanakushtukia....lakini wanajua Binti yao anakua na anavutia "waharibifu" na hivyo kesho yake wanaongeza Ulinzi, hakuna kwenda kwa Mangi(Dukani) peke yako, baada ya siku kadhaa unasahau kuwa uliahidi limjamaa jibu lake, kama unamkubali awe mpenzi wako ama la! Miezi inapita ukimuomba Mungu akuepushe usije kutana nae. Picha ya jamaa inaishia hapo.


Siku unatoka zako sehemu sehemu, mara unakutana nae tena, kwasababu ulisahau/dharau ahadi uliyoitoa unakuwa huna la kusema/mjibu na kiukweli huna mpango wa kuwa na mpenzi, unaanza kujieleza  kwanini ulimuacha solemba....anasikitika halafu bado anaomba jibu lake. Hapo unatamani ardhi ipasuke uingie, asikuone tena. 



Halafu kuna wale  wajanja ila wavivu, walijikuta Wamarekani wa Afrika eti walikuwa wanakutongoza kupitia Radio one sterioooooooo kipindi cha chombeza chombeza, unapatiwa dedication song hehehehe basi unajiskia special balaa japo huna mpango nae. !



Hii safari  ya kutongozwa na watu(wanaume) mbali mbali, kukataa, kutaka kukubali kwasababu unamdondokea lakini kama vile haupo tayari, maana kuna jamaa mwingine bora zaidi kuliko yeye pale kwanini upoteze maisha yako ya ujana kwa kuwa na mpenzi halafu uolewe halafu uzae kabla hata hujaishi maisha yako kama mwanamke, halafu pia wazazi hawatokuelewa na utawatia aibu ikitokea umeshika mimba kabla ya ndoa na vilevile hujui shughuli zake wala familia yake...too much, si bora ubaki single hyuu! ilikuwa ndefu na yenye usumbufu sana.


Hivi umewahi kuogopa kuwa na favorite child? au pengine you pray that wanao wasije kukushutumu kuwa unampendelea mmoja wao zaidi kuliko wao? Au ni pre-Menopause imeanza?😐

Bbai.

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao