Ukisema umefanya maamuzi mabaya ya kuruhusu huyo particular mtu maishani mwako nitakuelewa.
Kumbuka wewe ndio responsible kwa kila kinachotokea maishani mwako iwe ni maamuzi mazuri au mabaya.....beba mzigo na ujipange upya, sio kujipa-jipa moyo...eti sababu Mzungu anakuaminisha kuwa "people come in your life for a reason".
Kuna watu wanaishi ili kuharibu maisha ya watu, ndio furaha yao. Wengine walikosa mapenzi na malezi bora kutoka kwa Wazazi/Walezi matokeo yake wanayatafuta waliyoyakosa kwa kuharibu maisha ya wenzao.....nakadhalika.
Sasa ni juu yako kumsoma yeyote anaekuja maishani mwako na kumruhusu aingine kama Rafiki, Mpenzi, Jamaa ( wale mliooa/olewa Ukoo Mmoja), ukigundua tu kuwa umekosea basi haraka muepuke kabla hajaharibu zaidi.
Nikupe mfano?....I looooooooooove mifano hihihihihi(watu tunauelewa tofauti, bila mifano wengine tunatoka kapa).
Unaishi maisha Mzuri tu na Dada/Kaka yako, mnapendana, manashirikiana, saidiana na kushauriana.....Mtu pembeni anapenda maisha mnayoishi kama ndugu au familia. Yeye hana au hakuwahi kuwa karibu hivyo na Ndugu.
Anapiga mahesabu na kugundua kuwa njia pekee ni kuanzisha urafiki na Dada mtu, ili ampate kaka mtu kama Mpenzi kisha avuruge "undugu" wao kwa kuwa Mpenzi wa Kaka yako na hiyo inatakuwa furaha yake.
Mf wa Pili; Wale Wake/Waume wenza....kwamba mmeolewa Ukoo/Familia moja (hatari sana).....kwa vile wewe umeoa/olewa mwisho (kabla yao) kwenye Ukoo/Familia husika kwa kawaida unapata attention Mingi kuliko wale "wazee" hata kama Wadogo kwako bado walikuwepo kabla yako kwenye Ukoo/Familia hiyo.
Ili kuua attention au upendo unaoupata kutokana na Upya wako, wanaaza kuvuruga kwa kutumia njia zote zilizopo Chini ya Mbingu.
Mf wa Tatu na wa Mwisho; Mpenzi....baada ya safari zako zote unahisi hapo sasa ndio umefika mwisho wa Reli Kasuluuuuuu(is it?) Anyway! Yaani umependa.
Mpenzi anabadilika kutoka Mpenzi na kuwa Mtawala.....need I say more? Aiiiii Kimbia.
Hakuna ajae maishani mwako ili kukufunza au kukusijui nini na nini....wote unawaruhusu mwenyewe kwa Upumbavu au Ujinga wako au kutokuwa makini(unafanya maamuzi mabaya).
Hakuna mtu aliepita kwenye maisha yangu ambae kanifunza kitu, nikigundua wee ni "mzigo" aiii nakugaya....naanza Upya.....actually nafanya hivyo kila mwaka....maisha haya nani anataka mizigo ya stress?!!
Ya leo ndefu eti?
Pole....na babai.
Mapendo tele kwako...
Comments