Skip to main content

Mali ya Familia...

Kuna baadhi yetu tunatabia/kasumba ya kuita Mali za watu kuwa zetu na pengine kuanzisha fujo na kupelekea Vita kubwa ili kila mmoja apate "mgao" wake.


Kwasababu tu Mali ni za Baba/Mama yako au Kaka/Dada yako haikupi haki ya wewe kupata Mgao....wacha papara za kutaka kunijibu, nitakupa mfano ili unielewe vema.

Baba na Mama wameachana wakiwa hawana kitu, Baba kaanzisha uhusiano mwingine na kupata familia "mpya"....mambo yakaenda vema wakawa na Mali za kutosha....wewe uliezaliwa na Mama wa kwanza unadhani una unahaki na Mgao sawa kama watoto waliomo kwenye "familia Mpya"?


Upatikanaji wa Mali za Baba yako na familia yake Mpya unamchango Mkubwa wa Mama yao (familia Mpya) na sio Mama yako (alieachana na Baba yako akiwa hana kitu)....sehemu ya mali utakayoipata ni ndogo sana, tena kama Mke atakubali upatiwe. Mf; wa kwanza.

Mf wa Pili: Dada/Kaka kajipinda na kujituma yeye na Mume/Mkewe na sasa wanamiliki Mali nzito, inakuaje wakubwa/wadogo watu mhesabu kuwa hizo ni Mali za Familia wakati hakuna mchango wenu wala wa Baba na Mama yenu (Wazazi wenu)?


Hata kama umeajiriwa kwenye Kampuni ya Dada/Kaka bado Mali sio ya Familia....usifanye kazi bure ukitegemea kurithi Kampuni....dai Malipo(Mshahara) ili uweze kutengeneza Mali zako. Ukimfanyia ndugu yako tajiri kazi bure ni kwamba anakutumia....kwenye Maendeleo(kutafuta Pesa) hakuna Undugu, dai Malipo.

Wenzetu Wachaga (well naijua familia Moja tu hihihihi)hutumia "Chanzo" kimoja kupeana njia ya Maendeleo Mf: Bwana Shoo ana Duka, analeta mdogo wake....baada ya Miezi kadhaa nae anafungua Duka lake....analetwa mwingine, nae anatoka kivyake kupitia pale pale kwa Kaka....hakuna kungoja Mgao(Urithi).

Mali ya familia ni ile iliyotengenezwa na Mzazi wenu kisha kurithishwa kwa wengine ama waiendeleze kizazi hata kizazi au waiue(kila mtu apate chake afanya yake).


Wacha ku-relax ukiamini siku Dada/Kaka wakienda nitapata Mgao wangu...."Baba/Mama akienda nitapata Mgao wangu".


Jitume kwa jasho lako utengeneze zako, wacha kutegemea Urithi(Uzembe)....I say!

Babai.
Mapendo tele kwako...

Comments

Topic hizi tamba...

Weusi wa Kwapa na Vipele Makalioni....

Well Weupe huwa hawawi na weusi kwapani bali Unjano au Ukahawia....wale wenye nywele nyeusi sasa ni another case. Kuhusu Vipele makalioni havina Ubaguzi, raha ya vipele vile ni kwamba havionekani kwa Macho....utajua unavyo kwa kujipapasa, au gusa ngozi yako....inakuwa kama ina "mikwaruzo" wajua ile nanihii ya kupiga Msasa mbao? Yep ndio feels kama hivyo! Usione haya sio Ugonjwa na wala sio Tatizo kiafya, ni mambo ya Urembo tu na yawapata watu mbali mbali Ulimwenguni.....kama urembo sio issue kwako basi baki na Mapele yako na uyafurahie! Mimi nilikuwa nayo na siyapendi na ndio maana nataka nikupe mbinu ya "mapambano" ili uwage na Makalio "smooth"....Sasa hapa nikuambie kuhusu Vipele Makalioni au weusi wa Kwapa?.....Yote? Hamna shida twende in to them*. Vipele: Sijui inasababishwa na nini(sio mtaalam mie) ila nahisi ni kutoijali ngozi ya sehemu hiyo ndio inachangia....huisugui ukioga, huilainishi kwa mafuta, unavaa chupi za Mpira badala ya Pamba, huifanyishi

Kuachisha mtoto Kunyonya!

Heeeeeelp!!! Ka Binti kangu kana Mwaka na Nusu (Miezi18) lakini kamo tu, hata dalili ya kuacha hakana....Mie nimechoka kunyonyesha, nimechoka kuwa Mkubwa hapa Chini ya Kidevu bana! Babuu aliacha mwenyewe ghafla, yaani siku hiyo kaamka tu akagoma kunyonya....Mwanamke bembeleza, lazimisha mtoto wapi!!....alikuwa na Mwaka Moja na Mwezi(Miezi 13) na niliteseka Kihisia na Kimwili kwa Wiki nzima. Kihisia: Haina Uzungu hii, ila nililia sana....kwanini Mwanangu hataki kuwa karibu na mimi? (maana kunyonya kwake kulikuwa kunanipa ukaribu na Mwanangu). Nilipanga kumnyonyesha mpaka Mwaka na nusu (Miezi 18), kwanini Kanigaya(Susa) kabla sijawa tayari?!!! Kimwili: Matiti yanauma bwana asikuambie Mutu! Yalivimba(Jaa maziwa)....the more nakamua ndio yanajaa zaidi.....kamata simu Pigia Mama, Mama akasema "usiyakamue kwani ukikamua mwili wako unahisi mtoto anataka kunyonya zaidi so yanajitengeneza kwa Kasi ya ajabu". Kaongeza: "

Mashoga/Wasenge "wanatuibia" Waume/Wapenzi wetu....

...kwanza kabisa napenda utambue kuwa hakuna Mtu anaweza kumuiba  mwenzake kimapenzi, Mpenzi wako anapotoka kwako na kwenda kwa mwingine ni wazi kwamba kaamua kufanya hivyo, hilo sio kosa lako na wala hujasababisha yeye kwenda huko kwingine bali ni yeye mwenyewe na akili zake timamu kafanya uamuzi huo. Tangu Ushoga ndio khabari/Suala Muhimu wacha na mimi nidaivu ini nipate "trafiki" japo nimechelewa. Tofauti na "platform" nyingine hapa utajifunza kwa kiasi kidogo...au niseme kiasi fulani. Linapokuja suala la Ushoga/Usenge,sehemu kubwa ya Jamii imetawaliwa na  Uoga ambao unapelekea kutokuelewa Ushoga ni nini? Hali hiyo ni Asilia, kwamba mtu anazaliwa hivyo au ni uamuzi  wa mtu au ni Hali inayojitokeza ukubwani baada ya Kubalehe.....pale kijana anapoanza kutambua ujisia wake(je anavutiwa/penda Wanawake au Wanaume au wale wa Jinsi kama yake). Mie sio Mtaalam wa Masuala ya Kisenge/Shoga lakini ni mtu ambae napenda kudadisi, na watu wazuri kuwadadisi ni hao hao