Kwasababu tu Mali ni za Baba/Mama yako au Kaka/Dada yako haikupi haki ya wewe kupata Mgao....wacha papara za kutaka kunijibu, nitakupa mfano ili unielewe vema.
Baba na Mama wameachana wakiwa hawana kitu, Baba kaanzisha uhusiano mwingine na kupata familia "mpya"....mambo yakaenda vema wakawa na Mali za kutosha....wewe uliezaliwa na Mama wa kwanza unadhani una unahaki na Mgao sawa kama watoto waliomo kwenye "familia Mpya"?
Upatikanaji wa Mali za Baba yako na familia yake Mpya unamchango Mkubwa wa Mama yao (familia Mpya) na sio Mama yako (alieachana na Baba yako akiwa hana kitu)....sehemu ya mali utakayoipata ni ndogo sana, tena kama Mke atakubali upatiwe. Mf; wa kwanza.
Mf wa Pili: Dada/Kaka kajipinda na kujituma yeye na Mume/Mkewe na sasa wanamiliki Mali nzito, inakuaje wakubwa/wadogo watu mhesabu kuwa hizo ni Mali za Familia wakati hakuna mchango wenu wala wa Baba na Mama yenu (Wazazi wenu)?
Hata kama umeajiriwa kwenye Kampuni ya Dada/Kaka bado Mali sio ya Familia....usifanye kazi bure ukitegemea kurithi Kampuni....dai Malipo(Mshahara) ili uweze kutengeneza Mali zako. Ukimfanyia ndugu yako tajiri kazi bure ni kwamba anakutumia....kwenye Maendeleo(kutafuta Pesa) hakuna Undugu, dai Malipo.
Wenzetu Wachaga (well naijua familia Moja tu hihihihi)hutumia "Chanzo" kimoja kupeana njia ya Maendeleo Mf: Bwana Shoo ana Duka, analeta mdogo wake....baada ya Miezi kadhaa nae anafungua Duka lake....analetwa mwingine, nae anatoka kivyake kupitia pale pale kwa Kaka....hakuna kungoja Mgao(Urithi).
Mali ya familia ni ile iliyotengenezwa na Mzazi wenu kisha kurithishwa kwa wengine ama waiendeleze kizazi hata kizazi au waiue(kila mtu apate chake afanya yake).
Wacha ku-relax ukiamini siku Dada/Kaka wakienda nitapata Mgao wangu...."Baba/Mama akienda nitapata Mgao wangu".
Jitume kwa jasho lako utengeneze zako, wacha kutegemea Urithi(Uzembe)....I say!
Babai.
Mapendo tele kwako...
Comments